Wananchi wa kijiji cha Kurutu kilichopo kata ya Shungubweni wilayani Mkuranga mkoa wa Pwani wameshauliwa kuchukua shamba lenye ukubwa wa hekari 66.6 ambalo alipewa mwekezaji tangu mwaka 1988 na kushindwa kuliendeleza,ili walitumie Kwa shughuli za kuzalisha mali.
Ushauri huo ulitolewa wilayani humo na Mbunge wa jimbo hilo Mhe. Abdallah Ulega mara baada ya kupokea malalamiko kutoka Kwa wananchi wake akiwa katika ziara zake za kushukuru wanakijiji hao Kwa kumchagua kuwa mbunge wao.
Ulega alisema haiwezikani watu wanajimilikisha mashamba makubwa miaka hadi miaka alafu wanashindwa kuyaendeleza huku wananchi wakipata shida ya kukosa maeneo hata ya kulima kilimo cha mbogamboga vijana.
"Nasema kuwa kama shamba hilo limekaa miaka yote hiyo haliendelezwi, na pia huyo mwekezaji haonekani sasa mnasubiri nini kulichukua na kufanya uendelezaji. Nashauri litwaeni halafu tutapambana naye huko mbele"
Pia Ulega aliwaeleza wananchi hao kuwa siasa imekwisha na kilichobaki ni watu kufanya Kazi Kwa nguvu zote na kwamba atakuwa bega Kwa bega katika kuhakikisha maendeleo wanayapata Kwa haraka.
Awali wananchi wa kijiji cha Kurutu walimweleza mbunge kuwa wanavshamba kubwa ambalo alipewa mwekezaji miaka mingi iliyopita tena kienyeji lakini hadi leo ameshindwa kuliendeleza hivyo awasaidie walipate ili vijana wa eneo hilo wazalishe chumvi.
Mbunge huyo bado anaendelea na ziara zake za kutembelea kijiji hadi kijiji kwa lengo la kuwashukuru na kuhimiza shughuli za maendeleo ambapo anawataka kujituma katika kufanya kazi kwani wilaya hiyo imechelewa kimaendeleo.
Mbunge wa jimbo la Mkuranga Mhe Abdallah Ulega akielekea kijiji cha Kurutu kilichopo kata ya Shungubweni wilayani Mkuranga mkoa wa Pwani kwa mtumbwi.
Mbunge wa jimbo la Mkuranga Mhe. Abdallah Ulega akikagua daraja
Mbunge wa Jimbo la Mkuranga Mhe. Abdallah Ulega akizungumza na walimu wa shule ya msingi ya kijiji cha Kurutu kilichopo kata ya Shungubweni
Mbunge wa Jimbo la Mkuranga Mhe. Abdallah Ulega akizungumza na wananchi wa kijiji cha Kurutu kilichopo kata shungubweni wilayani Mkuranga katika ziara zake za kushukuru wanakijiji hao Kwa kumchagua kuwa mbunge wao.
Mwanakijiji Shabani Omary akiuliza swali kwa mbunge wa jimbo la mkuranga Mhe. Abdallah Ulega. Habari na picha na Emmanuel Masaka wa Globu ya Jamii
mbunge inabidi utijahidi kubuni njia za kunyanyua vipato vya wananchi wako kwani wanaoekana kuchoka kimaisha. hilo daraja linatia aibu fanya mchakato hela za jimbo zijenge darala la kueleweka.
ReplyDelete