Naibu
Waziri wa Maliasili na Utalii, Eng. Ramo Makani akizungumza na wananchi
katika viwanja vya Mwambisi Wilayani Kibaha Mkoa wa Pwani jana wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Kutundika Mizinga Kitaifa Mkoani humo. Naibu Waziri Makani ametoa wito kwa wananchi kutumia vizuri fursa ya maeneo ya misitu yaliyotengwa kwa shughuli za ufugaji nyuki kwenye ukanda wa wazi (buffer zone)
kwa kutundika mizinga mingi
na siyo kutumia maeneo hayo kwa shughuli nyingine za uharibifu wa
mazingira kama uchomaji mkaa kwa kuwa kufanya hivyo kutasadia uhifadhi
wa misitu na kuongeza uzalishaji bora wa mazao ya nyuki. Kulia ni Kaimu
Mkurugenzi wa Idara ya Misitu na Nyuki, Dkt. Ezekiel Mwakalukwa, Kaimu
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu, Prof. Dos Santos Silayo
(kushoto) na Mkuu wa Wilaya ya Kibaha, Asumpta Mshana (wa pili kushoto).
Naibu
Waziri wa Maliasili na Utalii, Eng. Ramo Makani (katikati) akizindua
Manzuki ya Makonga katika shamba la Miti Ruvu Kaskazini Wilayani Kibaha
Mkoa wa Pwani jana wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Kutundika Mizinga
Kitaifa yaliyofanyika Wilayani humo. Manzuki hiyo itatumiwa kama shamba
darasa la kuwaelimisha wananchi juu ya ufugaji wa nyuki kwa njia za
kisasa zitakazowezesha kuzalisha mazao bora ya nyuki. Kulia ni Kaimu
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania, Prof. Dos Santos
Silayo, Mkuu wa Wilaya ya Kibaha, Asumpta Mshana (wa pili kushoto) na
Katibu Tawala Mkoa wa Pwani, Daniel Isala (kushoto).
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Eng. Ramo Makani (kulia) akitundika mzinga wa nyuki katika
shamba la Miti Ruvu Kaskazini Wilayani Kibaha Mkoa wa Pwani jana wakati
wa Maadhimisho ya Siku ya Kutundika Mizinga Kitaifa Wilayani humo.
Kushoto anaeshiriki nae ni Mkuu wa Wilaya ya Kibaha, Asumpta Mshana na
kushoto kwa Mkuu wa Wilaya ni Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za
Misitu Tanzania, Prof. Dos Santos Silayo.
Naibu Waziri wa Maliasili, Eng. Ramo Makani (wa pili kushoto) akikagua miche ya miti katika shamba la miti Ruvu Kaskazini Wilayani Kibaha Mkoa wa Pwani jana wakati
wa Maadhimisho ya Siku ya Kutundika Mizinga Kitaifa yaliyofanyika
Mkoani humo. Shamba hilo lina jumla viriba vya miti milioni moja kwa
ajili ya kupandwa katika shamba hilo na maeneo mengine nchini. Kushoto
kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Kibaha, Asumpta Mshana, Kaimu Mtendaji Mkuu
wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania, Prof. Dos Santos Silayo (wa tatu
kulia) na Kaimu Mkurugenzi Idara ya Misitu na Nyuki, Dkt. Ezekiel
Mwakalukwa (kushoto).
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...