Aliyewahi kuwa Waziri wa elimu na Utamaduni katika
Serikali ya awamu ya tatu Mhe. Joseph Mungai (pichani), amefariki dunia leo majira ya
saa 11 jioni.
Akithibitisha taarifa hizo, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Umma katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Aminiel Aligaesha, alisema kuwa marehemu Mungai amefikishwa katika hospitali hiyo akiwa tayari amekwisha fariki na kwamba kwa upande wao hawajatoa matibabu yoyote zaidi ya huduma ya chumba cha kuhifadhia maiti (Mochwari)
"Ni kweli tumempokea Mungai, lakini alikuwa tayari amekwisha fariki, tunachosaidia sisi ni mochwari tu, kwahiyo kusema kuwa amefia Muhimbili siyo sahihi" Amesema Eligaesha.
Kuhusu chanzo cha kifo chake, Eligaesha amesema hadi sasa bado hakijafahamika, hadi uchunguzi utakapofanyika kwa kuwa hakufia katika hospitali hiyo. "Hatuwezi kusema nini chanzo hilo ni jukumu la familia, na pia kwa kuwa hajafia hapa hatuwezi kujua hadi postmoterm ifanyike, kwa sasa amehifadhiwa hapa" Alimalizia Eligaisha.
Mwili wa marehemu umehifadhiwa Chumba cha
maiti katika Hospitali hiyo ya Taifa ya Muhimbili. Habari kamili ya msiba
huo zitawajia kadri zitakavyokuwa zikitufikia. Mtandao huu unatoa pole kwa
ndugu, jamaa na marafiki.
Bwana ametoa na Bwana ametwaa, Jina la
Bwana lihimidiwe. Mungu ilaze roho ya Marehemu mahala pema peponi, Amina
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...