Katibu Mkuu Kiongozi Mwandamizi Kijazi (mwenye koti la bluu) akiongoza matambezi ya hiari sehemu ya maadhimisho ya siku ya Maadili nchini yatakayofikia kileleni tarehe 10 Desemba 2016 katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam na Matembeze hayo yamefanyika Leo jijini Dar es salaam kuanzia kwenye viwanja vya Karimjee na kufikia ukomo viwanja vya Mnazi Mmoja.
Katibu Mkuu Kiongozi Mwandamizi John Kijazi( mwenye koti la bluu) akishiriki katika mazoezi ya viungo baada ya kumaliza matembezi ya hiari ambayo yamefanyika Leo jijini Dar es salaam.
Katibu Mkuu Kiongozi Mwandamizi Balozi John Kijazi akiwahutubia washiriki wa matembezi ya hiari ( hawapo pichani) mara baada ya kumaliza matembezi hayo Jijini Dar es salaam.
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Profesa Musa Assad akizungumza mbele ya mgeni rasmi Balozi John Kijazi (hayupo Pichani) mara baada ya kumalizika kwa matembezi ya hiari katika viwanja vya Mnazi Mmoja na kushoto ni Katibu Mkuu wa Ikulu Peter Ilomo.
Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa ( TAKUKURU) ambaye ni mwenyekiti wa Kamati Kuu ya Maadhimisho ya Haki za Binadamu,Bw.Valentino Mlowola akifafanua jambo mara baada ya kumalizika kwa Matembezi ya Hiari yaliyomalizikia viwanja vya Mnazi Mmoja katikati ni Katibu Mkuu Balozi Kijazi.
You mixed up the two...
ReplyDelete