Mwendesha bodaboda akiiangalia Gari ndogo aina ya Toyota Raum yenye namba za usajili T 690 CMS iliyopata ajali usiku wa kuamkia leo katika eneo la Kiguza, Wilayani Mkuranga Mkoani Pwani. Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio la ajali hiyo, wanaeleza kuwa Gari hiyo iliyokuwa ikitokea upande wa Hoyoyo kuelekea Mkuranga, iliacha njia na kwenda kugonga mti uliokuwepo kando ya barabara hiyo, kwa madai ya dereva wake kushindwa kuona vizuri baada ya kumulikwa na taa kali (full light) ya gari iliyokuwa inakuja mbele yake. Hakuna aliyepoteza maisha kwenye ajali hii. 
Inavyoonekana gari hiyo baada ya kupiga mzinga.
Break Down au wazee wa kubeba visivyojiweza, wakiipiga cheni gari hiyo.
Picha na Emmanuel Massaka, Globu ya Jamii.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...