Kanisa la kiinjili la kilutheri Tanzania (KKKT) jimbo la Mufindi limekabidhi zaidi ya  shilingi milioni 02 kwa Mkuu wa wilaya ya Mufindi ikiwa ni sadaka maalum iliyotolewa na waumini wa kanisa hilo kwa wahanga wa janga la tetemeko la ardhi  lililotokea Mkoani Kagera mnamo septemba 13 mwaka huu. 
Taarifa ya kitengo cha habari na mawasilino cha halmashauri ya Wilaya ya Mufindi kwa vyombo vya habari, imeeleza kuwa, msaada huo wenye jumla ya shilingi  milioni 02 laki 02 na 52 elfu, umewasilishwa na mkuu wa jimbo la Mufindi mchungaji Anthony Kipangula wakati wa hafla fupi ya makabidhiano iliyofanyika katika Ofisi ya mkuu wa Wilaya Bomani mjini Mafinga.
Mchungaji Kipangula amesema wakati wa mkutano wao wa jimbo ulioketi  mapema mwezi oktoba, kwa kauli moja walikubaliana  kutoa  sadaka maalum kwa lengo la kusaidia waathirika  wa janga hilo kubwa na lakihistoria hapa nchini.
Akitoa shukrani mara baada ya kupokea misaada hiyo kwa niaba ya serikali, Mkuu wa wilaya ya Mufindi Jamhuri William, amewashukuru waumini wote waliojitoa kwa sadaka hiyo maalum kwa ajili ya waathirika wa Kagera na kuahidi kuikabidhi kwa Mkuu wa Mkoa, kisha akaziomba taasisi za dini ziendelee kuisadia serikali na jamii kwa ujumla katika masuala mbalimbali ya kijamii.
 Mkuu wa jimbo la KKKT la Mufindi mchungaji Anthony Kipangula (kati) akiongea na Mkuu wa wilaya ya Mufindi Jamhuri William (kushoto) wakati wa hafla fupi ya makabidhiano iliyofanyika katika Ofisi ya mkuu wa Wilaya Bomani mjini Mafinga.
Mkuu wa wilaya ya Mufindi Jamhuri William akishukuru kwa msaada huo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...