Mkuu wa Mkoa wa Singida Dr Rehema Nchimbi ametoa wito kwa watumishi wa Umma Mkoani humo kuingia mwaka 2017 wakiwa na uelewa sahihi wa malengo ya serikali ya awamu ya Tano ya kuwatumikia wananchi kwa uweledi na kutatua matatizo yao kwa kasi ili kuinua maisha ya wananchi na Maendeleo ya Mkoa huo.

Mwaka 2017,tunataka tupige hatua kubwa zaidi kupitia raslimali zetu ambazo zitawezesha maendeleo katika Mifugo, Ukulima Mazao ya Kisasa, Ufugaji Nyuki, Ufugaji Samaki, Uvunaji wa Maji ya Mvua, Utunzaji wa Mazingira na Usindikaji wa Mazao kwa malengo ya ujumla ya kumuendeleza mwananchi na kutosheleza mahitaji ya Wanasingida na Soko la Dodoma Makao Makuu ya Nchi. Tunafanikiwa iwapo wananchi wote, watendaji na Viongozi wote tutashirikiana na kuwajibika kwa uwaminifu, uwadilifu na uweledi. Aliongeza Dr Nchimbi

Dkt Nchimbi amewataka wanchi wote wa Mkoani Singida washerekee Mwaka Mpya kwa amani bila kufanya mambo yeyote yatakayo ashiria uvunjifu wa amani ili kuufanya Mkoa huo kuwa ni kielelezo cha Utulivyo na amani na kuwafanya wageni wanaoingia Singida wasiwe na hufu na masha juu ya usalama wao.

Nawashauri wananchi wa Mkoa wangu wa Singida kuukaribisha mwaka mpya kwa kwenda kwenye nyumba za ibada na kumshukuru Mungu kwa Uzima aliotupatia na pia kuombea Mkoa wetu wetu na Nchi kwa ujumla ili Mungu azidi kutukirimia neema zake, kwa wale watakao jaribu kuleta fujo napenda kuwaambia kuwa Jicho na Sikio la Serikali hapa Singida liko makini na watashughulikiwa kikamilifu. Alimalizia Mh Dr Nchimbi
Pichani ni Mkuu wa Mkoa wa Singida Dr Rehema Nchimbi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...