SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO)
linawatangazia wateja wake wa Mikoa ya Dodoma, Singida, Shinyanga, Tabora,
Mwanza, Geita, Mara, Simiyu
na na baadhi ya maeneo ya Mikoa ya Arusha,
Manyara, Kilimanjaro na
Tanga na baadhi ya maeneo ya Mkoa wa Dar es Salaam (Tazara, Mlimani City,
Mandela Road, Ubungo na Kimara, Sinza, Mabibo) kuwa yatakosa Umeme siku ya
Jumapili DESEMBA 04, 2016 kuanzia saa 02:00 Asubuhi hadi saa 11.00 Jioni.
SABABU: Kuruhusu Mkandarasi anayejenga Njia Kuu ya
Kusafirisha Umeme ya Msongo Mkubwa ya Kilovolti 400 maarufu kama (Backbone
Transmission Line 400 kV) kutoka Iringa hadi Shinyanga.
SABABU: Kuzimwa kwa njia ya
Umeme ya Msongo wa Kilovolti 33 Kituo cha Ubungo Dar es Salaam ili kumruhusu
Mkandarasi kufanya matengenezo yenye lengo la kuboresha na kuimarisha hali
ya upatikanaji wa Umeme Nchini.
Uongozi unaomba radhi kwa
usumbufu wowote utakaojitokeza.
Imetolewa na
Ofisi ya Uhusiano
TANESCO
Makao Makuu
Mhandisi wa umeme wa TANESCO akiwa kazini jijini Dar es Salaam
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...