Na Rhoda Ezekiel Kigoma,
BARAZA la Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko limemsimamisha kwa muda Diwani wa kata ya Gwalama Elia Kanjero (CHADEMA),kutohudhuria kikao kimoja cha Baraza la madiwani, kwa kosa la utovu wa nidhamu kwa baadhi ya Viongozi wa Serikali na Madiwani.


Adhabu hiyo ilitolewa jana katika kikao cha baraza la madiwani la halmashauri hiyo, ambapo Mwenyekiti wa halmashauri hiyo Juma Maganga alisema adhabu hiyo imetolewa na kamati ya maadili ya baraza hilo ili kujenga nidhamu kwa madiwani wengine kuwa na nidhamu kama viongozi wanao waongoza Wananchi.

Maganga alisema kosa moja wapo lilopelekea adhabu hiyo ni pamoja na Diwani huyo kwenda kutolea ufafanuzi katika kipindi cha kipimajoto cha ITV wa Rasimu ya kodi ya majengo ambayo ilikuwa haijapitishwa katika halmashauri hiyo na kudai sheria hiyo inayowakandamiza Wananchi bila kibali cha mwenyekiti wa Halmashauri hiyo.

Alisema Katika adhabu hiyo imeshuhudiwa na Mwenyekiti wa halmashauri pamoja na Katibu wake ambae ni Mkurugenzi wa halmashauri na Mtuhumiwa atakabidhiwa barua yake ya adhabu kupitia kwa Afisa utumishi wa halmashauri.

Kwa upande wake Diwani wa kata ya Gwarama Elia Kanjero(CHADEMA) alisema yeye kama kiongozi wa uponzani kuadhibiwa kwasababu ya Wananchi ni faraja kwangu na nitaendelea kuwatetea Wananchi kwa uwezo wangu na nitaitumikia adhabu hiyo.

Kanjero alisema kosa lililopelekea kuadhibiwa ni pamoja na kuwashawishi madiwani kupinga rasimu ya Wananchi kulipa kodi ya majengo pamoja na kwenda kutoa maoni dhidi ya kutoshirikishwa Wananchi katika Baadhi ya mambo yanayo endelea katika halmashauri, jambo ambalo sioni kama ni kosa la kunifanya niadhibiwe.

"Suala lingine lililopelekea Kuadhibiwa ni baada ya Mtendaji wa kata ya Garama kugushi saini yake na kusaini fedha za Mfuko wa maendeleo ya kata baada ya kuleta malalamiko kwa Mkurugenzi wamuhamishi ikawa chanzo cha Mimi kuonekana sina nidhamu suala ambalo nilikuwa nikipigania haki yangu na Wananchi walio nichagua",alisema Kanjero.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...