Na Nteghenjwa Hosseah, Arusha
Serikali Mkoani Arusha imesema busara ilipaswa kutumika zaidi katika Utekelezaji wa Agizo la Waziri Mkuu Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa alilotoa wakati wa ziara yake Wilayani Karatu katika Bonde la Eyasi kuhusu kusogezwa kwa Mashine za kuvuta maji Umbali wa Mita 500 kutoka chanzo cha Maji.
Katika Agizo lake Mhe. Waziri Mkuu aliagiza kusogezwa kwa mashine za za kuvuta maji kutoka chanzo cha maji cha bonde la Eyasi ambapo akati mchakato wa utekelezaji ukiendelea baadhi ya wakazi wa eneo hilo walizichoma moto mashine hizo ambazo kwa wakati huo zilikuwa zimesogezwa umbali wa mita 60 ambazo zinaruhusiwa kisheria.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo akiwa katika ziara ya Kikazi Wilayani Karatu amesema kutokana na umuhimu wa bonde la Eyasi katika uzalishaji wa Chakula haikuwa busara kwa wananchikuchoma mashine hizo bila kujali mazao ambayo tayari yameshaoteshwa katika eneo hilo na gharama zilizotumika kununua mashine hizo.
 Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo akizungumza na walimu wa wilaya ya Karatu katika siku ya kwanza ya ziara yake ya kikazi wilayani humo.
 Katika Kikao kingine Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho  Gambo (aliyesimama mbele) akizungumza na wazee wa Karatu pamoja na viongozi wa dini.
 Mtaalamu wa Halmashauri ya Karatu(kwanza kulia) akiwaandikisha  Wananchi wa Kijiji cha Oldeani waliojiunga na Mfuko wa afya ya Jamii wakati wa Mkutano wa hadhara na Mkuu wa Mkoa wa Arusha.
 Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo(kwanza kulia) akichangia Fedha kwa ajili ya wazee 10 kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii.  

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...