Katika kuendeleza juhudi za
kupunguza na kutokomeza majanga ya moto yanayoikabili jamii, Jeshi la Zimamoto
na Uokoaji limeendelea na zoezi la utoaji elimu juu ya Kinga na Tahadhari dhidi
ya Majanga ya Moto Nchini.
Jeshi la Zimamoto na
Uokoaji linajukumu kubwa la kutoa huduma kwa jamii katika Nyanja mbalimbali
zikiwemo Kuokoa maisha ya watu na mali zao, Kuzima moto, Kutoa elimu ya kinga
na tahadhari ya majanga moto, Kufanya ukaguzi wa tahadhari na kinga ya moto, Kusoma ramani za majengo na kutoa
ushauri, Kutoa huduma ya kwanza katika majanga na ajali barabarani, Kutoa
mafunzo ya kukabiliana na majanga ya moto, Kufanya uchunguzi kwenye majanga ya
moto na Kutoa huduma za kibinadamu.
Huduma ya Zimamoto
inatolewa bure na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji hivyo basi tunawaasa wananchi
kutumia namba ya dharura 114 mara tu wapatwapo na majanga ili kurahisisha
uokoaji wa Maisha na Mali kwa haraka.
Kwa kuzingatia majukumu
hayo Askari wa kituo cha Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Mbeya wamewapatia
elimu ya kukabiliana na majanga ya moto Watumishi wa banki ya Access tawi la
Mkoa wa mbeya.
Sajini Simon Sadala wa kituo cha Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Mbeya (Mbele) akitoa elimu ya Kinga na Tahadhari dhidi ya majanga ya moto katika taasisi ya kifedha(Access Bank) tawi la Mbeya.
Askari wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa mbeya wakiwa kwenye picha ya pamoja na Watumishi wa benki ya Access tawi la mbeya mara baada ya kumaliza kupata mafunzo hayo mapema leo asubuhi (Picha na Jeshi la Zimamoto)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...