JANUARY 16, 2017 — MJI MKONGWE,  ZANZIBAR:  Harakati za kukamilisha taratibu za ushiriki wa kikundi cha Yamoto Band hazikufanikiwa kutokana na changamoto za ugumu wa mawasiliano baina ya uongozi wa kikundi hicho na Uongozi wa Sauti za Busara. Sauti za Busara  imesitisha taratibu za kuruhusu ushiriki wa kikundi cha Yamoto Band kwenye tamasha la mwaka huu kama ilivyotangazwa awali.
Yusuf Mahmoud, Mkurugenzi wa tamasha amesikitishwa na ugumu wa kufanya mawasilaino ndani ya muda husika kutengeneza mazingira mepesi ya uandaaji wa taratibu zote za kuhakikisha kikundi hicho kinakamilisha mahitaji yote ndani ya muda uliopangwa.

“Kuna vipaji vingi sana vya muziki Tanzania.  Vipaji hivi hufifia kwa sababu ya uhaba wa ujuzi kwa mameneja ambao hawajibu barua pepe, wanakataa kusaini mikataba, hawafiki kwenye mikutano hata baada ya kuthibitisha kuwa watashiriki, na hawapokei simu,’’ Yusuf alikaririwa akisema hayo wiki iliyopita kwenye gazeti la Sunday News.

Journey  Ramadhan, Meneja wa tamasha amesema kuwa jitihada za makusudi za kuhakikisha  Yamoto Band wanashiriki tamasha hazikuzaa matunda baada ya yeye kufika Dar es Salaam na kumsubiri meneja wa Yamoto Band afike kwa ajili ya maongezi lakini alisema yuko nje ya mji  na asingeweza kuonana naye.

“Ili kuibua, kung’arisha  na kukuza vipaji vya muziki Tanzania tunahitaji mameneja wenye kuheshimu mawasiliano yatakayowezesha wanamuziki kupata nafasi ya kuonesha vipaji vyao kupitia wadau wa muziki nchini. Pia ni vema msanii apate naasi ya kushiriki kwenye matamasha ya kimataia ni lazima aanye mawasiliano kwa njia ya kieletroniki,’’ amesema Ramadhan.

Uzoefu wa kufanya kazi na mameneja wa wanamuziki  tofauti hapa nchini unaonesha ugumu wa kupokea simu, kushindwa kujibu barua pepe, kuhundhuria kwenye mikutano baina ya wadau wa muziki ili kujadili njia sahihi za kuhakikisha wasanii wanapata nafasi ya ushiriki ni changamoto kubwa zinazorudisha nyuma harakati za kukuza muziki Tanzania, amesema Ramadhan.

Yusuf ametoa wito kwa wasanii na mameneja wao kutumia tamasha la SzB  ambayo ni nafasi pekee  na sahihi ya  kutangaza na kuonesha kazi zao na kupanua wigo wa kung’arisha taaluma zao na kuongeza mawasiliano na wasanii na wadau wa muziki  kutoka sehemu mbali mbali duniani ambao hukutana kwenye tamasha hilo la siku nne mfululizo.

   

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...