Mkuu wa mkoa wa Mbeya Mh.Amos Makalla akiagiza vyumba vya wafanyabiashara vilivyofungwa na halmashauri vifunguliwe mara moja,na kuwarejeshea Wafanyabiashara kwenye meza ya mazungumzo na kuiondoa kesi baraza la Ardhi , RC Makala pia ametoa siku saba kwa Mkurugenzi wa halmshauri hiyo amalize Mgogoro wa kodi kwa kukaa meza moja na wafanyabiashara.

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makalla amefanya ziara katika mji wa Mbalizi kwa kutembelea kituo cha mabasi na soko la mbalizi na baadaye kufanya mkutano wa hadhara na wafanyabiashara na wananchi wa mji wa Mbalizi.

RC Makala pia alipata wasaa wa kusikiliza kero mbalimbali za Wafanyabiashara na Wananchi kwa ujumla,kufuatia malalamiko na kero za wafanyabiashara hao,RC Makala amemuagiza Mkurugenzi na baraza la Madiwani kuhakikisha ndani ya siku saba mvutano wa kodi ya pango la vyumba sokoni hapo uwe umekwisha kwa kupatiwa ufumbuzi.

Aidha RC Makala pia amesikitishwa kwa namna ambavyo Mgogoro huo umeachwa kwa muda mrefu bila kushughulikiwa na kusababisha mvutano mkubwa na kupelekea halmashauri kushtakiwa kwa baraza la Ardhi

Rc Makala ameagiza uongozi wa halmashauri na Mamlaka ya mji Mdogo wa Mbalizi kusimamia usafi.Wananchi na wafanyabiashara wameshukuru na kupongeza uamuzi wa Mkuu wa Mkoa na wameahidi kuitoa kesi hiyo Mahakamani na kukaa katik meza ya mazungumzo na halmashauri kumaliza mvutano wa pango la Vibanda vya biashara.
Baadhi ya wakazi na wafanyabishara wa soko la Mbalizi wakitoa kero zao kwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya alipo fanya ziara katika Stendi ya Mabasi na Soko la Mbalizi Mkoani Mbeya.
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mh.Amos Makalla akihutubia wananchi katika mkutano wa hadhara na wafanyabishara na wananchi wa Mji mdogo wa Mbalizi Mkoani Mbeya.HABARI PICHA NA MR PENGO-MMG MBEYA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...