Katika kuhakikisha inaboresha huduma kwa wafanyabiashara ambao wanaingiza mizigo nchini kwa njia ya bandari, mipaka na viwanja vya ndege, Serikali kupitia Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) imeeleza mpango wa Serikali wa kuanza kutumia mfumo wa Dirisha Moja la Huduma (Electronic Single Window System) ambao kwa hakika utamaliza tatizo la mizigo kukaa muda mrefu kwa sababu ya kukosekana vibali.
Akizungumza
na waandishi wa habari baada ya kumalizika mafunzo ya siku moja kuhusu
mfumo wa Dirisha Moja la Huduma kwa taasisi zinazotoa vibali na
wafanyabiashara, Meneja Mfumo wa Kieletroniki wa Dirisha Moja la Huduma,
Tinka Felix alisema lengo la kuanza kutumia mfumo huo ni kuboresha
huduma ambazo wanazitumia sasa ili wafanyabiashara wanaoingiza mizigo
nchini waweze kuipata kwa haraka kuliko ilivyo sasa.
Meneja Mfumo wa Kieletroniki wa Dirisha Moja la Huduma, Tinka Felix akizungumza kuhusu mfumo wa Dirisha Moja la Huduma (Electronic Single Window System). (Picha zote na Rabi Hume - MO DEWJI BLOG)
“Ni mpango wa Serikali kuboresha huduma kwa wateja kwa kupunguza muda wa kutoa mizigo bandarini au mipakani au kwenye viwanja vya ndege, kupitia mfumo huu wateja hawatakuwa wakienda kwenye idara na taasisi za Serikali na badala yake wakiwa hukohuko kwenye ofisi zao wataweza kuomba na kupata vibali na kupata bili za malizo kwenda kulipa benki, mfumo pia utafanya kazi na benki," alisema Felix.
Meneja Mfumo wa Kieletroniki wa Dirisha Moja la Huduma, Tinka Felix akizungumza kuhusu mfumo wa Dirisha Moja la Huduma (Electronic Single Window System). (Picha zote na Rabi Hume - MO DEWJI BLOG)
“Ni mpango wa Serikali kuboresha huduma kwa wateja kwa kupunguza muda wa kutoa mizigo bandarini au mipakani au kwenye viwanja vya ndege, kupitia mfumo huu wateja hawatakuwa wakienda kwenye idara na taasisi za Serikali na badala yake wakiwa hukohuko kwenye ofisi zao wataweza kuomba na kupata vibali na kupata bili za malizo kwenda kulipa benki, mfumo pia utafanya kazi na benki," alisema Felix.
Alisema
Tanzania haitakuwa nchi ya kwanza kutumia mfumo huo na mataifa mengi
yanautumia ili kurahisisha huduma kutolewa kwa haraka kwani mfumo wa
sasa wa forodha (tancis system) unashindwa kufanya kazi kwa haraka jambo
ambalo linasababisha mizigo kuchelewa kutolewa kutokana na muda mrefu
mmiliki kutumia kutafuta vibali. Mkurugenzi
wa Sera Utafiti Na Ushauri wa TPSF, Gili Teri akizungumza faida za
kutumia mfumo wa Dirisha Moja la Huduma (Electronic Single Window
System).
“Mfumo wa sasa ili mtu apate kibali anatakiwa atembelee hizo ofisi hata mara 10 na baadhi ya ofisi wanataka vibali zaidi ya kimoja lakini mfumo huu wa sasa muda ambao unatumika kuomba vibali utapungua na tunategemea kuokoa Dola milioni 65 kwa kutumia tu mfumo wa electronic single window system,” alisema Felix.
“Mfumo wa sasa ili mtu apate kibali anatakiwa atembelee hizo ofisi hata mara 10 na baadhi ya ofisi wanataka vibali zaidi ya kimoja lakini mfumo huu wa sasa muda ambao unatumika kuomba vibali utapungua na tunategemea kuokoa Dola milioni 65 kwa kutumia tu mfumo wa electronic single window system,” alisema Felix.
Alisema
kwa sasa kuna taasisi za Serikali 47 ambazo zinatoa vibali lakini mfumo
wa Dirisha Moja la Huduma utatumiwa na taasisi 32 ambazo kwa pamoja
zitakuwa zikitoa vibali 106. Aidha alisema Serikali imeagiza kuwa mfumo
huo uanze kutumika baada ya mwaka mmoja hivyo wanategemea kuanzia
mwakani mfumo ambao watakuwa wakitumia utakuwa ni wa Dirisha Moja la
Huduma (Electronic Single Window System) ambao utawezesha
wafanyabiashara ambao wanatoa mizigo kupitia bandari, mipaka au viwanja
vya ndege kupata vibali kwa haraka.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...