Ushauri umetolewa kwa Shirikisho la Mpira wa miguu nchini (TFF) kuangalia namna ya kuwaendeleza wachezaji wanaohudhuria kliniki ya wiki moja ya Airtel Risingf Stars inayofanyika kwenye uwanja wa Jakaya Kikwete Youth Park jijini Dar es Salaam.

Ushauri huo umetolewa na Kocha Msaidizi wa timu ya Taifa ya Wanawake ya Twiga Stars Edna Lema ambaye ni moja kati ya makocha wanaotoa mafunzo kwa wachezaji hao ambao walichanguliwa kutokana na michuano ya awamu ya sita ya Airtel Rising Stars.

Tuna wachezaji wazuri na wenye vipaji vya hali ya juu na kliniki hii inadhirihisha hivyo. Kwa wachezaji hawa kuendelea na vipaji vyao ni lazima kuwe na mipango endelevu. Kinachofanyika kwa sasa ni kwamba baada ya kliniki hii, wachezaji wataruhusiwa kurudi makwao mpaka pale tutakapokuwa na michuano ya kimataifa ndio tuanze kuwatafuta bila kujali huko walikokuwa walikuwa wanafanya nini. Bila kubadilisha hali hiyo ni vigumu kwa timu zetu kupata mafanikio, alisema Lema.
Tuliendea kufanya ziara nchini Cameroon na kushuhudia mipango yao ya kuendeleza vipaji. Kwao wanakuwa na kliniki za kudumu za wachezaji wa rika zote. Kwa kuwaweka wachezaji pamoja ujenga hali ya ukaribu kati yao pamoja na makocha pia na kwa hali hiyo sio ajabu kwa nchi hiyo kuwa kwenye michuano ya Kombe la Dunia na hile ya Afrika. Natoa wito kwa TFF kubadilisha jinsi ya kutunza wachezaji wetu kuleta mafanikio kwenye timu zetu za taifa, aliongeza Lema.

Akiongelea kuhusu kliniki ya Airtel Rising Stars, kocha huyo Msaidizi wa Twiga stars alisema anaamini timu ijayo itakuwa na vipaji vya hali ya juu. Wachezaji hawa ni wazuri sana, ukipewa jukumu ya kuchangia timu inaweza kuwa mtihani umchukue yupi na kuwacha yupi. Kwakweli tunafurahi kupata vipaji hivi kutoka kwenye mashindano haya.

Lema alitoa pongezi kwa kampuni ya Airtel kuwa na program hii ya vijana ambayo kwa mwaka jana iliweza kufika mikoa tisa ya Tanzania. ‘Hii ndio njia bora na sahihi ya kupata wachezaji wa timu zetu, alisema Lema.

Mmoja ya wasichana wanaoshiriki kwenye kliniki hiyo Eva Willes alisema anayo furaha ya kuwa mmoja ya washiriki wa kliniki hiyo. Kwa muda mrefu nimekuwa nikicheza mpira wa miguu na nilikuwa na ndoto ya kuwa mchezaji wa timu ya taifa. Kuwepo kwenye kliniki kunanifungulia milango ya kutimiza ndoto zangu. Nitaendelea kuongeza bidii pamoja na kuwasikiliza makocha kwa makini nipate mafanikio zaid, alisema Willes.
Kocha Mkuu wa Timu ya Wasichana U-17, Sebastian Nkoma akitoa maelekezo kwa wachezaji wa timu hiyo wakati wa Kliniki ya Airtel Rising Stars yanayofanyika katika Uwanja wa Jakwaya Kikwete Dar es Salaam jana kutafuta vijana wenye vipaji kuunda Timu ya Taifa.
Kocha Msaidizi wa Timu ya Wasichana ya Twiga Stars, Edna Lema akitoa maelekezo kwa wachezaji wa timu hiyo wakati wa kliniki ya Airtel Rising Stars yanayofanyika katika Uwanja wa Jakwaya Kikwete Dar es Salaam jana kutafuta vijana wenye vipaji kuunda Timu ya Taifa.
Wachezaji wa Timu ya wasichana U-17, wakifanya mazoezi katika Uwanja wa Jakaya Kikwete wakati wa Kliniki ya Airtel Rising Stars Dar Salaam jana kutafuta vijana wenye vipaji kuunda Timu ya Taifa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...