#LakeFm Habari
Wakazi wanaoishi maeneo ya mijini nchini wamehimizwa kujikita kwenye kilimo cha mbogamboga kwa kutumia masalia ya makopo na mifuko ya aina mbalimbali ili kuondokana na uchafunzi wa mazingira.

Mwanamama Victoria Buzare ambaye ni mjasiriamali kutoka Kata ya Buhongwa Jijini Mwanza, ameyasema hayo wakati akizungumza na Lake Fm huku akiongeza kwamba kilimo hicho pia kinawaepusha wanajamii na athari za kutumia mbogamboga zenye kemikali.

Amesema kilimo hicho kinagharimu mtaji kidogo hadi shilingi 5,000 ambazo mkulima anaweza kulima aina tatu za mbogamboga ikiwemo sukumawiki, nyanya chungu, biringanya na nyinginezo.

Buzare amewashauri wanafamilia wote wanaoishi mijini kuhakikisha wanakuwa na bustani za makopo na mifuko kwani ni salama kwa matumizi ya chakula na pia rahisi kusimamia ikizingatiwa ndoo moja ya maji kwa siku inatosheleza mahitaji yake.
Kwa maoni na ushauri ama swali, wasiliana na Victoria Buzare (pichani) kwa nambari za simu 0754 21 85 55.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...