Waziri
wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage akizindua Jiwe la
Msingi la Kiwanda Keds.kwakushirikina na Mkurugenzi wa Kiwanda hiko, Jack
Feng.
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji,
Charles Mwijage ameweka jiwe la msingi kuashiria kuanza kwa ujenzi wa
Kiwanda cha Sabuni (Keds) kilichopo Kibaha Mkoani Pwani.
Kiwanda hicho ni cha pili kujengwa katika Bara la Afrika baada ya cha kwanza kujengwa nchini Ghana.
Akizungumza wakati wa uwekaji wa jiwe hilo,Waziri
Mwijage amesema kuwa amefurahi kuona mapambano yakuendeleza Tanzania ya
Viwanda,amesema kupitia ujenzi wa Viwanda hivyo ukuaji wa Uchumi utakuwa
sambamba na ukuaji wa Maendeleo ya Watu.
Pia amesema kuwa Kiwanda hiko cha Keds kimeitoa
Tanzania kimasomaso katika kutimiza asilimia 40 ya upatikanaji wa ajira
pamoja na kuziomba Mamlaka za Mikoa kote nchini kuiga Mfano wa Pwani
katika Uwekezaji wa Viwanda na kujifunza ukarimu kwa wawekezaji.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha
Uwekezaji nchini (TIC),Clifford Tandari amesema kuwa ni fursa muhimu kwa
kuwa Kampuni hiyo tayari ina Kiwanda Ghana hivyo kujengwa Tanzania
kitakuwa cha pili.
Amesema kuwa baada ya Kiwanda hicho kuisha kitaokoa gharama za uingizaji wa sabuni kutoka nje.
Naye Mkurugenzi wa Kiwanda hiko, Jack Feng,amesema
tangu kuanza kwa mradi huo wametumia muda mfupi kuweka sawa ardhi ya
eneo hilo pia amesema kuwa watajenga kwa uzoefu na ujuzi ili kutimiza
azma ya uwekezaji bora Tanzania.
Waziri
wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage akizungumza wakati
wa uwekaji wa jiwe la msingi kuashiria ujenzi wa Kiwanda cha Keds
kilichopo Kibaha Mkoani Pwani.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Nchini, Clifford Tandari akizungumza
wakati wa uwekwaji wa jiwe la msingi katika Kiwanda cha Sabuni cha Keds.
Mkurugenzi wa Kiwanda hiko, Jack Feng akizungumza wakati wa uwekwaji wa jiwe la msingi katika Kiwanda cha Sabuni cha Keds.
Baadhi
ya viongozi mbalimbali na wanachi wakimsikiliza Waziri wa
Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage wakati wa uwekaji wa
jiwe la msingi kuashiria kuanza kwa ujenzi wa Kiwanda cha Sabuni(Keds) kilichopo
Kibaha Mkoani Pwani.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...