Mbunge wa Jimbo la Chato na Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani (aliyevaa miwani) akizungumza na wananchi wa kijiji cha Nyakayondo kuhusiana na utekelezaji wa miradi mbalimbali kijijini humo na jimboni kwa ujumla.
Mbunge wa Jimbo la Chato na Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani akielekeza jambo wakati wa ukaguzi wa kisima (kilichofunikwa kwa nyasi) kilichochimbwa katika kijiji cha Nyakayondo. Jumla ya visima virefu 30 vinatarajiwa kuchimbwa jimboni humo.

Mbunge wa Jimbo la Chato na Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani (kushoto) akiongozana na Mkuu wa Wilaya ya Chato, Shaban Ntalambe (kulia) na Diwani wa kata ya Bwanga, Nuhu Mahmoud (katikati) wakati wa ukaguzi wa ujenzi wa vyumba vya madarasa na ofisi ya walimu katika shule ya Msingi ya Bwanga B. Mradi huo unahusisha ujenzi wa vyumba vitano vya madarasa, ofisi ya walimu na matundu 30 ya vyoo.
Mbunge wa Jimbo la Chato na Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani (wa pili kushoto) akielekeza jambo wakati wa ukaguzi wa utekelezaji wa miradi mbalimbali jimboni humo. Kulia ni Mhandisi wa Maji wa Wilaya ya Chato, Mhandisi Mali Misango. Nyuma ya Dkt. Kalemani ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Chato, Christian Manunga. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...