Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Maji na Umwagiliaji, itakuwa mwenyeji wa Maadhimisho ya 11 ya ‘Siku ya Nile’ yatakayofanyika Dar es Salaam, tarehe 22 Februari, 2017.

Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa kushirikiana na Sekretariati ya Nile Basin Initiative (NBI) itaandaa Maadhimisho ya 11 ya Siku ya Nile (Nile Day) yatakayofanyika tarehe 22 Februari, 2017 katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.
Lengo la Siku ya Nile ni kukuza uelewa kwa watu wote kuhusu umuhimu wa ushirikiano baina ya nchi zote wanachama, masuala yanayotekelezwa na faida inayopatikana kutokana na matumizi bora ya rasilimali za Bonde la Mto huo. 
Kauli Mbiu ya Maadhimisho hayo ni ‘Our Shared Nile: Source of Energy, Food and Water for All’. Kauli mbiu hii inalenga kuonesha umma umuhimu wa Mto Nile katika kuhakikisha usalama wa upatikanaji wa chakula, maji, na nishati ya umeme kwa jamii nzima na vilevile, kuonesha muingiliano uliopo katika sekta husika kwa lengo la kuondoa umasikini, kuboresha maisha ya jamii na kuleta maendeleo endelevu. 
Mgeni rasmi wa maadhimisho hayo atakuwa ni Mhe. Samia Suluhu Hassan, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Washiriki takribani 600 watashiriki maadhimisho hayo zikiwemo sekta mbalimbali, taasisi za kiserikali, taasisi zisizo za kiserikali, wadau wa

maendeleo na watu mashuhuri. 

Maadhimisho yanatarajiwa kuanza saa 02:30 asubuhi, siku ya tarehe 22 Februari, 2017 kwa maandamano yatakayo ongozwa na Bendi ya Polisi kuanzia viwanja vya Mnazi Mmoja hadi Ukumbi wa Kimataifa wa Julius Nyerere, ambapo maonesho na ufunguzi rasmi wa maadhimisho hayo yatafanyika.

KARIBUNI SANA!

Inj. Emmanuel Kalobelo
KAIMU KATIBU MKUU
Wizara ya Maji na Umwagiliaji

20 Februari, 2017

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...