Waziri wa Mambo ya Katiba Na Sheria Dkt. Harrison Mwakyembe ameagiza kuwa kuanzia tarehe 1 Mei, 2017 ndoa zote zifungwe baada ya wanaotaka kufunga kuwasilisha kwa vyeti vya kuzaliwa kwanza.
Hivyo, amewataka wananchi wote wanaotarajia kufunga ndoa waanze kutafuta vyeti vya kuzaliwa mapema kwa sababu hawataweza kufunga ndoa kuanzia tarehe 1 Mei, 2017.
Agizo hilo amelitoa kwa Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) leo tarehe 16/3/2017 akiwa ziarani mkoani Morogoro kukagua utendaji wa taasisi zilizo chini ya Wizara ya Mambo ya Katiba na Sheria.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...