Waziri mstaafu Profesa Mark Mwandosya akiwa ameamka alfajiri na mapema ili kufanya mazoezi na kuzunguka katika ziwa Nyasa hususan kwenye fukwe maarufu na mwanana za Matema wilayani Kyela mkoani Mbeya. Fukwe hizo ni mojawapo ya vivutio vikubwa vya utalii kwa kuwa na mandhari ya kupendeza, samaki wa kila aina pamoja na utengenezaji wa vyungu, magudulia na mitungi vya udongo. Profesa Mwandosya ameiambia Globu ya Jamii kwa njia ya mtandao kwamba Matema Beach pia ni location nzuri sana kwa watengeneza filamu za muziki, tamthiliya na kadhalika.
Waziri mstaafu Profesa Mark Mwandosya akiwa anafurahia Matema Beach
Waziri mstaafu Profesa Mark Mwandosya akiwa anafurahia Matema Beach ndani ya mtumbwi unaoteleza juu ya maji tulivu na masafi ya Ziwa Nyasa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...