Pamoja na jitihada zinazofanyika kuhakikisha kuwa na vyumba maalum kwa ajili ya watoto wa kike kujisitiri wanapokuwa katika hedhi lakini bado changamoto kubwa ni upatikanaji wa vitambaa wakati wa hedhi "pedi"kwa watoto wa kike hasa kwa watoto wasio na uwezo.

Hayo yamebainika wakati wa ziara ya waandishi wilayani Kishapu walipotembelea shule mbalimbali kuangalia hali ya upatikanaji wa vyumba kwa ajili ya kujisitiri watoto wa kike wanapokuwa katika hedhi na upatikanaji wa vitambaa ‘pad’ ili kuimarisha usafi wa mtoto wa kike anapokuwa shuleni.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti walimu wa wakuu wa shule za msingi na walimu walezi wa wanafunzi wa kike wilayani Kishapu walisema wamejitahidi kuwa na vyumba maalumu kwa ajili ya watoto wa kike kujistiri wanapokuwa kwenye hedhi lakini changamoto ni upatikanaji wa pad kwani watoto wengi hawana uwezo wa kununua pedi.

Walisema shule nyingi hazina uwezo wa kifedha kuweza kununua pedi na kuzigawa bure kwa wanafunzi hivyo kuwaomba wadau mbalimbali wa watoto kujitokeza kusaidia watoto wa kike kwani wazazi wengi wamekuwa wakidai hawana uwezo wa kununua vitambaa hivyo.

Vyoo vya wanafunzi (kushoto) na cha walimu (kulia) katika shule ya msingi Nyenze iliyopo katika kata ya Mwadui Lohumbo wilayani Kishapu
Choo cha wanafunzi katika shule ya msingi Nyenze ambacho kina chumba kimoja maalum kwa ajili ya wanafunzi wa kike kinachotumiwa na wanafunzi hao wanapokuwa katika hedhi
Chumba maalumu kwa ajili ya watoto wa kike/wanafunzi wa kike wanaosoma katika shule ya msingi Nyenze.Pamoja na kuwepo kwa chumba hicho lakini hakuna kifaa chochote kwa ajili ya watoto wa kike wanapokuwa katika hedhi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...