Na Bakari Madjeshi, Globu ya Jamii
Wakala wa Vipimo nchini imewaasa Wajasiriamali kuzingatia Vipimo sahihi katika upimaji wa bidhaa ili kuendana na Uchumi wa Viwanda na kufikia soko la Kimataifa kwa bidhaa husika.
Akizungumza na Globu ya Jamii katika Maonyesho ya Kimataifa ya Wanawake Wajasiriamali yaliyojumuisha nchi za Tanzania,Rwanda, Burundi, Uganda na Comoro, Kaimu Meneja, Elimu, Habari na Mawasiliano-Wakala wa Vipimo, Irene John amesema kuwa wafanyabiashara wote watumie matumizi sahihi ya vipimo wanapotumia au kufungasha bidhaa zao.
Irene amesema kuwa si sahihi wafanyabiashara kutumia vikombe, Kopo au Debe  badala ya Mzani katika upimaji wa bidhaa,amebainisha kuwa ni kinyume cha Sheria ya Vipimo, Sura namba 340 mapitio ya mwaka 2002(Faini ya Sh. 10,000) na Maboresho ya sheria ya mwaka 2016 faini  ni  Sh. 100,000 au kifungo cha Mitatu au vyote kwa pamoja.
Kwa upande wao Wajasiriamali waliohudhuria Maonyesho hayo,Grady John na Glory Shayo wamewashukuru Wakala wa Vipimo kutoa elimu kwa Wajasiriamali hao kutokana kuwafanya wateja wa bidhaa hizo kuwa na uhakika kutokana na vipimo sahihi.
Kaimu Meneja, Elimu, Habari na Mawasiliano-Wakala wa Vipimo, Irene John akitoa Elimu ya Vipimo kwa Mjasiriamali na Msimamizi wa Mafuta ya Dina Marios Baby Oils, Glory Shayo katika Maonyesho ya Kimataifa ya Wanawake Wajasiriamali jijiniDar es salaam

 Kaimu Meneja, Elimu, Habari na Mawasiliano-Wakala wa Vipimo, Irene John akizungumza na Mwandishi wa Michuzi TV kuhusiana na elimu kwa Wajasiriamali kutumia Vpimo sahihi katika upimaji wa bidhaa.

 Mjasiriamali na Msimamizi wa Mafuta ya Dina Marios Baby Oils, Glory Shayo akielezea bidhaa hiyo katika Maonyesho ya Kimataifa ya Wanawake Wajasiriamali jijiniDar es salaam
Sehemu ya Wafanyabiashara waliohudhuria Maonyesho ya Kimataifa ya Wanawake Wajasiriamali yaliyojumuisha nchi za Tanzania,Rwanda, Burundi, Uganda na Comoro.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...