Naibu Inspekta Jenerali wa Jeshi la Polisi nchini, D-IGP Abdulrahman Kaniki (katikati) akiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Huawei Tanzania, Gaomeng Dong (kushoto) wakikata utepe kuashiria uzinduzi wa makabidhiano ya pikipiki 20 zilizotolewa na Kampuni ya Huawei kwa Jeshi la Polisi nchini zitakazosaidia katika shughuli mbalimbali za kukabiliana na uhalifu hapa nchini. Pikipiki hizo ni sehemu ya pikipiki 56 zilizokuwa zimeahidiwa na Kampuni hiyo kwa Jeshi la Polisi ili ziweze kusaidia ufanisi wa kazi kwa Jeshi hilo.
Naibu Inspekta Jenerali wa Jeshi la Polisi nchini, D-IGP Abdulrahman Kaniki akiwa amepanda kwenye moja ya pikipiki hizo alipokuwa akiijaribu, muda mfupi baada ya kukabidhiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Huawei Tanzania, Gaomeng Dong (wa pili kushoto) katika hafla fupi ya makabidhiano hayo, iliyofanyika katika viwanja vya Polisi Oysterbay, Kinondoni jijini Dar es salaam leo.
Naibu Inspekta Jenerali wa Jeshi la Polisi nchini, D-IGP Abdulrahman Kaniki akizungumza katika hafla hiyo.
BOFYA HAPA KUONA PICHA ZAIDI
BOFYA HAPA KUONA PICHA ZAIDI
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...