Timu ya soka ya Mbeya City imepata mfadhili mpya wa timu hiyo ambaye atakuwa anasimamia maswala yote ya vifaa vya michezo ikiwemo jezi zote za timu hiyo zitakazotumiwa na wachezaji na zile za mashabiki kuanzia mwezi wa saba mwaka huu. Viongozi hao wamesaini mkataba wa udhamini huo uliofanyika katika ukumbi mdogo wa hoteli ya Mbeya Hill View kwa kuwaalika wadau wa mbeya city na vyombo vyote vya habari.
Mwenyekiti wa Timu ya Mbeya City, Mussa Mapunda (kushoto) akipokea mkataba kutoka kwa Kiongozi wa Sports Master ambao ni wadhamini wapya watakaosimamia maswala yote ya vifaa vya michezo vya Timu hiyo, Fadhili Nsemwa, baada ya kusainiana makubaliano.
Mwenyekiti wa Timu ya Mbeya City, Mussa Mapunda akisaini mkataba wa makubalino na uongozi wa Kampuni ya Sports Master chini yake Fadhili Nsemwa (kulia).
Mfano wa Vifaa vya michezo vitakavyotumiwa na Timu ya Mbeya City kuanzia msimu ujao.
Picha ya pamoja.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...