Naibu Waziri ofisi ya Makamu wa Raisi muungano na Mazingira Mheshimiwa Luhaga Mpina, amewataka wakazi wa Mkoa wa Morogoro kutunza Vyanzo vya maji na Mazingira kwani kwa kufanya hivyo watakuwa wameokoa maisha ya binadamu na viumbe hai wengine.
Naibu Waziri Mpina ameyasema hayo leo alipikuwa katika zoezi la usafi kitaifa Mjini Morogoro ambapo amesisitiza kwa kufanya hivyo wakazi wa mkoa huo watakuwa wamesaidia wakazi wa Mkoa wa Dar es Salaam Pamoja na pwani ambao vyanzo vyao vyingi vya maji vimetokea mkoani Morogoro.
Mpina pia aliweka msisitizo katika zoezi zima la upandaji miti ambapo kila wilaya inatakiwa kupanda miti milioni moja na nusu, "kutakuwa na ufuatiliaji wa hali ya katika utekelezaji wa zoezi hiyo katika ngazi ya Wilaya." Alisisitiza Mpina.
Aidha Mpina aliunga Mkono Jitihada za Mkuu wa Mkoa wa Morogoro katika suala zima la utunzani na usafi  wa mazingira , "Mnae Mkuu wa Mkoa anaetosha, anaujua mkoa vizuri na hwa ndiyo viongozi wa mkoa tunaowataka, wachapakazi na wenyekujituma. Alisema Mpina."
Akiongelea suala la kuhamishwa wananchi katika milima na vyanzo vya maji, NW Mpina Alisema kuwa  " Tunapowaondoa wananchi katika maeneo hayo aimaaninishi kwamba tunawatesa. tunawapenda ndo maana tunawahamishia katika maeneo salama na rafiki kwa mazingira, RC watoeni wananchi wanaokaa katika maweneo Hatarishi." Alisema.
Kwa Upande wake Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Bwana Kebwe Steven Kebwe, akizungumzia hali ya mazingira ya mkoa huo, alisema kuwa mkoa utajitahidi kupambana na hali ya uharibifu wa mazingira, pamoja na changamoto mkoa unazokumbana nazo akitolea mfano upungu wa vifaa vya kuzolea taka.

Jumamosi ya usafi wa Mazingira Mkoani Morogoro kwa Jumamosi ya Mwishho wa mwezi wa nne ni utegelezaji wa Agizo la Mhe. Rais la Usafi wa Mazingira. 
 Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina akitoa Mchanga katika moja ya Mtaro Mijini Morogoro wakati wa kufanya usafi, Leo.
Moja ya Mtaro Uliosafishwa katika zoezi la usafi wa mazingira leo Mjini Morogoro

 Kulia Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Bwna Kebwe Steven Kebwe akimkabirisha Naibu Waziri Mpina kabla a kuanza kwa zoezi la Usafi kitaifa Mjini Morogoro siku ya Jumamosi ya Mwisho wa mwezi wa nne.
(Habari na Picha na Evelyn Mkokoi wa OMR)
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...