Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli akiwa katika gari maalum na kuwapungia mkono Wananchi mbali mbali wa Mji wa Dodoma wakati wa sherehe za miaka 53 ya Muungano wa Tanzania zilizofanyika leo katika Uwanja wa Jamhuri. Kulia kwake ni Mkuu wa Majeshi Jenerali Venance Salvatory Mabeho.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiwasili kwenye sherehe za Miaka 53 ya Muungano katika Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma. 
Kulia kwake ni Mkuu wa Majeshi Jenerali Venance Salvatory Mabeho.
Vikosi vya Jeshi la Wananchi wa Tanzania JWTZ, pamoja na Wananchi mbali mbali wa Mji wa Dodoma wakiwa katika Uwanja wa Jamhuri,wakati wa sherehe za maadhimisho ya miaka 53 ya Muungano wa Tanzania zilizofanyika leo,Mgeni rasmi akiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli.
Baadhi ya Wananchi waliohudhuria katika sherehe za maadhimisho ya miaka 53 ya Muungano wa Tanzania katika Uwanja wa Uhuru zilizofanyika leo,ambapo Mgeni rasmi akiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli.Picha na Ikulu.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na mjane wa Rais wa kwanza wa Zanzibar Mama Fatma Karume pamoja na mjane wa Baba wa Taifa Mama Maria Nyerere kwenye sherehe za Miaka 53 ya Muungano katika Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kwenye sherehe za Miaka 53 ya Muungano katika Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akipeana mikono ya pongezi na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein kwenye sherehe za Miaka 53 ya Muungano katika Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na walioshiriki katika zoezi la kuchanganya udongo kuasisi Muungano wa Tanganyika na Zanzibar kwenye sherehe za Miaka 53 ya Muungano katika Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma. Wananchi hao ni Bw. Hassan Omary Mzee (hayupo pichani), Bw. Hassaniel Elisael Mrema (kushoto), Bi. Sifael Kunda Shuma (anayepewa mkono) na Bi. Khadija Abbas Rashid 
Gadi ya “Komando” la vijana likiwajibika kwenye sherehe za Miaka 53 ya Muungano katika Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma.
Onesho la ndege vita kwenye sherehe za Miaka 53 ya Muungano katika Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma 
Onesho la mbwa wa polisi kwenye sherehe za Miaka 53 ya Muungano katika Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma 
Onesho la Komandoo wawili kuvuta lori la tani 7 kwa mikono kwenye sherehe za Miaka 53 ya Muungano katika Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma.
Kikosi cha Komandoo cha  JWTZ kikitoa heshima kwenye sherehe za Miaka 53 ya Muungano katika Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma


PICHA NA IKULU

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...