Na Tiganya Vincent, RS-Tabora

Katibu Tawala Mkoa wa Tabora(RAS) Dkt. Thea Ntara amewataka Wachimbaji Wadogo wadogo waliopo eneo la Kitunda wilayani Sikonge kuzingatia matumizi mipira ya kufanyia mapenzi(condom) wanapoamua kufanya hivyo ili kujikinga na maambukizi yanayowekusababishia kupata Virusi vya UKIMWI.

Hatua hiyo itasaidia waweze kuendelea kuwa na afya nzuri itakayowasaidia kuishi maisha mengi na kukatiza ndogo zao.
Dkt. Ntara alitoa kauli hiyo jana wilayani Sikonge wakati akitoa pole kuifuatia Maafa ya wachimbaji Saba wa madini katika eneo la Kitunda ambapo sita walikufa kwa kufukiwa na kifusi na mmoja alikufa kwa kukosa hewa.

Alisema kuwa umati wa wachimbaji ulipo katika eneoi hilo ni zaidi ya elfu kumi, hivyo ni vema wakatumia mipira kujikinga na UKIMWI wakati wakifanya mapenzi ili uwepo dhahabu hapo usije ukasababisha tatizo lingine katika jamii hiyo na ile inayowazunguka.

Dkt. Ntara alisema kuwa wachimbaji wengi katika eneo hilo bado wanaumri mdogo hivyo ni vema wakalinda afya zaidi ili wasiweze kutumbukia katika matatizo yatakayokazi maisha yao na kupoteza nguvu kazi ya Taifa ambayo bado inahitajika sana kwa maendeleo ya nchi hii.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...