Serikali ya Mkoa wa Songwe imeanza kuchukua hatua madhubuti kwa lengo la kupambana na changamoto zinazotokana na maambukizi mapya ya Virusi vya Ukimwi ili kuweza kufikia malengo ya taifa baada ya kuanza kutekeleza mwongozo mpya wa matibabu kwa wote wanaogundulika na VVU kuanzia Oktoba 2016.

Hayo yamesemwa leo na Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Songwe Ndg. Eliya Ntandu katika hotuba yake iliyosomwa na Mkuu wa Wilaya ya Mbozi Mhe. John Ernest Palingo kwenye kikao cha wadau wa afya kilicholenga kutambulisha mradi unatoa huduma mbalimbali za kupunguza maambukizi ya ukimwi ujulikanao kama SAUTI unaofadhiliwa na shirika la Misaada ya Kimataifa ya Maendeleo la Marekani(USAID) na kutekelezwa na shirika la Jhpiego.

Akielezea Mradi wa SAUTI katika Mkoa wa Songwe, Mhe. Palingo amesema anatambua malengo ya mradi huu kuwa ni kusaidia jitihada za serikali katika kuboresha afya za wananchi na kupunguza maambukizi ya Virusi vya Ukimwi ambapo mkoa wa Songwe ni wanufaika wakubwa kupitia wilaya mbili za Mbozi na Tunduma ambako mradi huu unatekelezwa.

“Mradi huu utasaidia sana kupunguza hatari za maambukizi ya Ukimwi katika makundi maalum yenye hatari zaidi ya kuambukiza au kuambukizwa VVU hususani wanawake wanaoanya biashara ya ngono, Vijana wa Kike nje ya shule walio katika mazingira tete kama ilivyoanishwa katika mwongozo mpya wa serikali wa 2017 unaosimamia huduma za VVU na Ukimwi kwa makundi maalum” alisema Mhe. Palingo
Mkuu wa Wilaya ya Mbozi Mhe. John Ernest Palingo akifungua kikao cha wadau wa afya Mjini Songwe kilicholenga kutambulisha mradi unatoa huduma mbalimbali za kupunguza maambukizi ya ukimwi ujulikanao kama SAUTI unaofadhiliwa na shirika la Misaada ya Kimataifa ya Maendeleo la Marekani(USAID) na kutekelezwa na shirika la Jhpiego.
Mkurugenzi wa mradi wa SAUTI Dkt. Albert Komba akiwasilisha mada kuhusu Mradi wa Sauti ambao ni Mradi wa miaka mitano unaofadhiliwa na Shirika la Misaada la Marekani (USAID) kupitia Mpango wa dharura wa raisi wa Marekani kwa ajili ya UKIMWI (PEPFAR) katika kikao cha wadau wa afya kwa lengo la kuutambulisha mradi huo.
Mratibu wa kudhibiti Ukimwi kutoka TACAIDS katika Mkoa Songwe Ndg. Emanuel Petro akiwasilisha mada kuhusu mikakati ya Mkoa katika mapambano dhidi ya virusi vya UKIMWI, Mafanikio na changamoto katika kikao hicho.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...