Tiganya Vincent, RS-Tabora

 Wananchi wa Mkoa wa Tabora wanakwenda kuona wagonjwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Kitete wameondokana na adha ya muda mrefu ya kunyeshewa mvua na kukaa juani baada ya kukamilika na kuzinduliwa kwa Jengo la Mahali pa Kungonjea kuona wagonjwa.
 
Jengo hilo lililojengwa na Ofisi ya Katibu Tawala Mkoa wa Tabora na umegharimu shilingi milioni 18 hadi kukamilika.
 
Uzinduzi huo umefanywa leo na Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Tabora Queen Mlozi wakati wa sherehe fupi zilzofanyika katika Hospiali ya Rufaa ya Mkoa huo Kitete.
 
Alisema kuwa kukamilika  kwa jengo hilo kwa muda kumesaidia kuondoa kilio cha muda mrefu cha viongozi na wananchi cha kutaka lijengwe eneo la watu kupumuzika wakati wakisubiri muda wa kuona wagonjwa wao wanapata matibabu katika Hosptali hiyo.

Kaimu Mkuu huyo wa Mkoa wa Tabora aliipongeza Seketarieti ya Mkoa wa Tabora kwa kuwa wabuni hadi kufanikisha ujenzi huo kwa kiwango cha juu na gharama nafuu.
 
Naye Katibu Tawala Mkoa wa Tabora Dkt. Thea Ntara alisema kuwa ujenzi wa jengo hilo umefanywa kwa kutumia fedha za usimamizi wa miradi ambapo Seketarieti ya Mkoa huo imepunguza katika fedha zake za kufuatilia miradi.
 
Alisema kuwa hatua hiyo imesaidia kupatikana kwa fedha hizo zilizosaidia kukamilisha kwa jengo ambalo ambalo litasiadia kuepusha wananchi hao na hatari za kugongwa na baiskeli au pikipiki kutokana na kukaa kando kando ya barabara.
 
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...