Na Othman Khamis, OMPR
 AmeMakamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi amewasili Zanzibar akitokea Mjini Amman, Jordan, alikohudhuria Jukwaa la tisa la Dunia la Uchumi (World Economy Forum) la Siku Tatu lililohudhuriwa na zaidi ya Wajumbe 2,000 kutoka Nchi 58 Duniani. 
Balozi Seif alimuwakilisha Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli kwenye Jukwaa hilo la Kanda ya Mashariki ya Kati na Kaskazini mwa Afrika lililoshirikisha Viongozi Wakuu wa Nchi, Wafanyabiashara,wamiliki wa Makampunni ya Kimataifa, 
Wawakilishi wa Taasisi za Kiraia, Mashirikia ya Kimataifa, Wana Habari pamoja naVijana wapatao 2,000. 
 Katika Mkutano huo wa Jukwaa la Dunia la Uchumi Balozi Seif na Ujumbe wake alishiriki Washa ya Utalii iliyojikita zaidi katika masuala ya Kujenga Uchumi kwa Mataifa yaMashariki ya Kati na yale ya Kanda ya Afrika ili kuona njia gani zinaweza kutoa fursa za ajira kwa Vijana kwa kutumia Teknolojia ya Kisasa Mkutano huo wa Jukwaa la Uchumi Duniani ulifunguliwa na Kiongozi wa Jordan Mfalme wa Pili Abdullah Bin Al-Hussein kwenye Ukumbi wa Kimataifa wa King Hussein Bin Talal katika Bahari Nyeusi. 
 Jukwaa la Uchumi la Dunia  limeasisiwa Mwaka 1971 chini ya Muanzilishi na Mwenyekiti wake Profesa Klaus Schwab huko Davos, Switzerland.
 Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akisalimiana na baadhi ya Mawaziri na Watendaji Wakuu wa Serikali mara alipowasili kwenye uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Abeid Aman Karume akitokea Nchini Jordan kushiriki Mkutanowa Jukwaa la Dunia la Uchumi akimuwakilisha Rais wa Jamuhuri ya Mauungano wa Tanzanmia Dr. John Pombe Magufuli.
Balozi Seif  Kushoto akibadilishana Mawazo na Baadhi ya Mawaziri wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika chumba cha Watu Mashuhuri (VIP) kongwe. Picha na OMPR, ZNZ.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...