Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Dr. Idrisa Muslim Hija amelishauri Shirika la Taifa la Biashara Zanzibar (ZSTC) na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kuangalia uwezekano wa kuanzisha taasisi maalum itakayoshughulikia tafiti za kitaalamu juu ya zao la karafuu.
Alitoa ushauri huo wakati akizungumza na Wakulima na Wadau wa zao la karafuu katika mkutano maalum ulioandaliwa na Shirika la ZSTC kwa Wakulima na wadau wa zao hilo Mkoa wa Kusini Unguja.
Alisema kutokana na zao la karafuu kuendelea kuwa uti wa mgongo wa uchumi wa nchi na wananchi wake ambapo wananchi wengi wanaonyesha nia na ari ya kulima zao hilo hivyo wanahitaji msaada mkubwa wa kitaalamu juu ya ukulima wa zao hilo.
 Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Dr. Idrisa Muslim Hija akimkabidhi kitambulisho cha ukulima wa zao la karafuu Mmoja kati ya wakuliwa wa zao hilo.
Baadhi ya Wakulima wa zao la karafuu Mkoa wa Kusini Unguja wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Mkoa huo. Habari kamili BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...