MKUU
wa wilaya ya Ikungi mkoani Singida Miraji Mtaturu amekutana na kamati
ya mfuko wa elimu wilaya na kuwaomba kuwa wazalendo katika kutafuta njia
za kutatua changamoto za elimu wilayani humo.
Mfuko huo umeundwa baada ya uanzishwaji wake kuridhiwa na kikao cha baraza la madiwani kilichoketi hivi karibuni.
Akizungumza
katika kikao cha kuwapatia majukumu yao Mtaturu amesema mfuko huo
utakuwa na jukumu la kuratibu masuala yote yatakayosaidia kuboresha
utoaji wa elimu katika shule za msingi na sekondari.
“nawapongezeni
kwa heshima mliyopewa ya kuteuliwa kuwa wajumbe wa kamati hii,naimani
kuwa mtafanya kazi kwa uzalendo mkubwa ili matunda ya uwepo wenu
yaonekane kwa kuitoa elimu yetu hapa ilipo na kuipeleka mbali
zaidi,”alisema Mtaturu.
Alisema
wakifanikiwa kuondoa changamoto zilizopo watakuwa wameboresha mazingira
ya utoaji elimu na kuongeza ufaulu wa watoto jambo ambalo waliazimia
walipokutana wadau wa elimu.
Mkuu wa Wilaya Ikungi Miraji Mtaturu katikati akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa kamati ya mfuko wa elimu wilaya ns viongozi wa halmashauri baada ya kumaliza kikao nao.
Mjumbe mwakilishi wa madhehebu ya dini sheikh Salum Ngaa akichangia hoja wakati wa kikao kilichoongozwa na mkuu wa wilaya ya Ikungi Miraji Mtaturu pichani wakiwa na wajumbe wa kamati ya mfuko wa elimu wilaya.
Kaimu mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Ikungi Haika Massawe akichangia hoja wakati wa kikao cha wajumbe wa kamati ya mfuko wa elimu wilaya.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...