Umoja wa Wakulima wa Ndimu wa Kikundi cha Juhudi Zetu kilichopo Bwejuu, mjini Unguja wametoa kilio chao cha kukosa soko la ndimu wanazozalisha kwa uongozi wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB).
Wakizungumza na ugeni huo, wakulima hao wamesema kwa muda mrefu sasa wamekosa soko la uhakika la mazao yao kwa kukosa mnunuzi wa uhakika licha ya kulima kisasa na kupata mazao mengi.
Mmoja wa wakulima hao Bw. Shafi Hamadi Mussa amesema kuwa kwa muda mrefu sasa wamekosa soko la uhakika la mazao ya hali inayorudisha nyuma ari ya kuendelea kulima zao hilo.
“Tunakatishwa tamaa kwa kukosa soko la uhakika licha uwekezaji mkubwa tunaoufanya katika kulima kisasa,” Bw. Mussa alisema.
Bw. Mgana Khatibu Mgana, mkulima mwengine wa Umoja huo amesema changamoto ya ukosefu wa masoko inaweza kutatuliwa kwa kupatiwa mkopo nafuu wa kununulia mitambo ya uchakataji wa mazao ambayo itatumika kuongeza thamani kwa mazao yao.
 Ugeni kutoka Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) wakikagua mashamba ya midimu wakati walipotembelea mashamba ya Umoja wa Wakulima wa Ndimu wa Kikundi cha Juhudi Zetu kilichopo Bwejuu, mjini Unguja.
 Ugeni kutoka Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) wakikagua mashamba ya midimu wakati walipotembelea mashamba ya Umoja wa Wakulima wa Ndimu wa Kikundi cha Juhudi Zetu kilichopo Bwejuu, mjini Unguja.
 Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Francis Assenga (kulia) akioneshwa miundombinu ya umwagiliaji ya kilimo cha ndimu. Anayemuonesha ni Bw. Mgana Khatibu Mgana na (kushoto) na Bw. Kombo Haji Mussa (katikati).
 Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Francis Assenga (kulia) akiangalia namna midimu inavyomwagiliwa maji.
Meneja wa Mikopo wa TADB, Bw. Samuel Mshote (kushoto) akiangalia ndimu zilizoanguka kwa kukosa wateja. Kwa mujibu wa wakulima wa ndimu, ndimu huuzwa ikiwa katika hali ya kijani lakini changamoto za kukosa soko hupelekea ndimu za wakulima wa Kijiji cha Bwejuu kuivia mtini. Kwa taarifa kamili BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...