NA BALTAZAR MASHAKA, MWANZA

KAMISHNA Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Charles Kichere amewahamasisha wananchi wenye majengo katika Jiji la Mwanza kuhakikisha wanalipa kodi ya majengo kwa wakati ili kuepuka kutozwa faini au kufikishwa mahakamani.

Akizungumza na waandishi wa habari pamoja na wadau wa kodi jijini Mwanza jana Kichere alisema kodi ya majengo ipo kwa mujibu wa sheria na italipwa mara moja kwa mwaka, hivyo ni muhimu wananchi wakailipa mwaka huu wa fedha kabla ya Juni 30 .

Alisema TRA haina sababu ya kufikishana mahakamani an wananchi lakini watakaoshindwa kulipa ndani ya muda wa kisheria watalazimika kulipa na tozo au kufikishwa mahakamani na kulingana na matakwa ya sheria za mamlaka hiyo watalipa sh. 70,000 badala ya viwango vya sh. 20,000 (Nyamagana) na sh. 15,000 (Ilemela) vya sasa.

“ TRA na Serikali ya Mkoa wa Mwanza inalenga kuwaelimisha na kuwahamasisha wananchi kulipa kodi hii bila adhabu ifikapo Juni 30, mwaka huu ambayo ni mwisho.Wenye majengo kwenye Halmashauri ya Jiji na Manispaa ya Ilemela ambao hawajapokea Ankara zao za kodi wakazichuke ofisi za TRA au kwa viongozi wa serikali za mitaa yao ama wajisajili na kulipia benki yoyote ya biashara,”alisema Kichere.

Alisema TRA mkoa wa Mwanza inasimamia kodi ya majengo yaliyokamilika na kutumika kwa makazi na biashara yaliyothaminishwa au la,yaliyopimwa na yasiyopimwa katika Halmashauri ya Jiji la Mwanza pamoja na Manispaa ya Ilemela.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongella akizungumzia umuhimu kodi ya majengo kwenye mkutano wa wadau wa kodi uliofanyika Ukumbi wa Ofisi yake.Kulia kwake ni Kamishna wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Charles Kichere, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Kamishna wa Polisi Cloudwing Mtweve na wa kwanza kulia ni Richard Kayombo Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi makao makuu TRA.Picha zote na BALTAZAR MASHAKA
Mkuu wa mkoa wa Mwanza John Mongella akielezea umuhimu wa wananchi kulipa kodi ya majengo kwenye mkutano wa wadau wa kodi uliofanyika katika Ukumbi wa Ofisi yake.Kulia kwake ni Kamishna wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Charles Kichere, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Kamishna wa Polisi Cloudwing Mtweve na wa kwanza kulia ni Richard Kayombo Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi makao makuu TRA.
Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Charles E. Kichere akizungumza na wadau wa kodi pamoja na waandishi wa habari jijini Mwanza kuhamasisha ulipaji kodi ya majengo kwa wakati bila shuruti.Watatu kutoka kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongella, Katibu Tawala mkoa, CP Cloudwing Mtweve (wa pili kulia) naRichard Kayombo,Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi makao makuu TRA wa kwanza kulia , kushoto wa kwanza ni Ernest Dundee,Meneja wa mamlaka hiyo mkoani humu .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...