Spika wa Bunge Mhe Job Ndugai leo ameendelea kuwaadhibu wabunge ambao wamekwenda kinyume na taratibu na ukosefu wa nidhamu baada ya kumuamuru Mbunge wa Kibamba , Mhe. John Mnyika wa CHADEMA kutoka nje ya bunge kwa utovu wa nidhamu.
Spika Ndugai aliamuru walinzi wa Bunge kumtoa nje mbunge huyo na kusema hataruhusiwa kushiriki katika vikao vya bunge kwa siku 7, jambo ambalo limepelekea wabunge wengine wa upinzani kutoka nje ya ukumbi wa Bunge kupinga kitendo hicho.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...