.
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
Mwenyekiti wa Cha Soka Mkoa wa Mara (FAM) Michael Wambura amechukua fomu ya kugombea nafasi ya makamu wa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini (TFF).
Wambura anakuwa kiongozi wa kwanza kuchukua fomu kugombea nafasi ya makamu wa rais wa TFF . Michael Wambura aliwahi kuteuliwa katika kamati ya utendaji ya Simba na aliyekuwa Rais wa klabu hiyo Ismail Aden Rage.
Wambura amewahi kuwa katibu mkuu wa Simba na ndiye alikuwa mtu wa kwanza kumshinda Rage katika nafasi ya ukatibu mkuu wa Chama cha Soka Tanzania (FAT)
Mwenyekiti wa Cha Soka Mkoa wa Mara (FAM) Michael Wambura akionesha fomu ya kugombea nafasi ya makamu wa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini (TFF)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...