Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Simon Sirro, akizungumza na askari wa Jeshi hilo wakati alipofanya ziara ya kikazi katika mkoa wa Shinyanga, IGP Sirro, amewataka askari kutimiza wajibu wao wa kuwatumikia wananchi kwa kutenda haki na kuzingatia sheria na taratibu.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Shinyanga, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Simon Haule (aliyesimama), akitoa hotuba mbele ya Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Simon Sirro, ambaye yupo mkoani humo kwa ziara ya kikazi yenye lengo la kuzungumza na askari na maofisa wa Jeshi hilo.
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Simon Sirro, akizungumza na baadhi ya wananchi wa mkoa wa Shinyanga, waliojitokeza barabarani msafara wake wakati akitoka kuzungumza na askari na maofisa wa Jeshi hilo, IGP Sirro, amewataka wananchi hao kuendelea kuitunza amani na kushirikiana na Jeshi la Polisi katika kuwavichua wahalifu.
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Simon Sirro (kulia), akimsikiliza kamanda wa Polisi mkoa wa Tabora, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Wilbroad Mutafungwa, aliyekutananae wakati akiwa safarini kuelekea mkoa wa Singida kwa ajili ya muendelezo wa ziara yake ya kikazi ya kujitambulisha na kuzungumza na askari wa Jeshi hilo. Picha na Jeshi la Polisi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...