William Henry Gates III maarufu kama Bill Gates na Mwanzilishi wa kampuni ya Microsoft iliyomfanya kuwa mtu tajiri namba moja duniani na mwanzilishi wa mashirika lukuki yasiyo ya kiserikali yenye kusaidia jamii yupo nchini. Leo ametembelea kijiji cha Kicheba wilayani Muheza katika mkoa wa Tanga kwa lengo la kuangalia maswala mbalimbali ya afya ikiwemo utumiaji wa dawa za mabusha, matende ili kuangalia ni namna gani anaweza kusaidia kwenye sekta hiyo ya Afya.
Mkuu wa wilaya ya Muheza Mkoani Tanga, Mhandisi, Hajat Mwanasha Tumbo (kushoto) akiwa na Bill Gatesbpamoja na mmoja wa viongozi wa kinamama wa wilaya hiyo katika kata ya Kicheba Wilayani humo mkoani Tanga leo
Bill Gates akiwasili na kusalimiana na uongozi wa wilaya ya Muheza katika kata ya Kicheba Wilayani humo mkoani Tanga leo. Kujua mengi kuhusu Bill Gates BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...