RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein, amesema kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itaendelea kutoa huduma zote muhimu kwa wananchi wake zikiwemo huduma za afya bila ya ubaguzi.

Dk. Shein aliyasema hayo leo, huko Junguni, Wilaya ya Wete, Mkoa wa Kaskazini Pemba mara baada ya kuzindua Kituo cha Afya cha Mama na Mtoto, ikiwa ni muendelezo wa ziara yake kiswani Pemba.

Katika maelezo yake Dk. Shein alisema kuwa kamwe Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar haitombagua mtu yoyote kwa itikadi yake ya kisiasa na badala yake itahakikisha wananchi wote Zanzibar wanapata huduma muhimu za maendeleo.

Dk. Shein alisema kuwa mwananchi yeyote anaekwenda kituoni hapo kupata huduma za afya hatabaguliwa kwani yeye ni mwananchi wa Zanzibar na akiwa mzazi atazalishwa kwa kufuata taratibu zote kwa mujibu wa taaluma aliyosomeshwa na Serikali.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...