BAADA ya baadhi ya vyombo vya habari kutangaza kuwepo mgogoro kati ya wananchi na serikali katika Pori tengefu la Mkungunero wilayani Kondoa mkoa wa Dodoma, mkuu wa wilaya hiyo amejitokeza na kudai taarifa hizo hazina ukweli.


Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana, Mkuu wa Wilaya ya Kondoa Bibi Sezaria Makota, alisema habari zilizosambazwa kuhusiana na wananchi kunyanyaswa katika pori la Mkungunero zinazungumzia matukio ya zamani ambayo kimsingi yameshapatiwa ufumbuzi na serikali.



“Katika taarifa zilizotolewa kwenye vyombvo vya habari imeelezwa kuwa viongozi na wanakijiji katika Kijiji cha Kisondoko na Kata ya KK kuwa wananyanyaswa na kuna wasichana walisema wamebakwa lakini nakanusha taarifa hizi si za kweli, wafanyakazi wa pori la Mkongonero wanajiheshimu na wanafanya kazi kwa nidhamu,” alisema Bi. Makota na kuongeza:



“Nilipofika Kondoa mwaka jana (2016) nilisikia hayo malalamiko lakini nilipofuatilia nikabaini si kweli, viongozi wa kamati ya ulinzi na usalama waliitisha mkutano kuwahoji wanakijiji wanaosema walinyanyashwa, kupigwa na kubakwa, kulikuwepo na madaktari waliowafanyia vipimo lakini hakuna aliyeonekana amebakwa.”




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...