MSHINDI
Mkuu wa mchezo wa bahati nasibu ya Tatu Mzuka , Rashid Ally, leo
amekabidhiwa sh.milinoni 80 alizojishindia katika droo kubwa
iliyochezwa Jumapili.
Rashid
ambaye alijishindia kiasi hicho cha fedha katika mchezo huo wa Tatu
Mzuka, alionyesha kutoamini, huku akiwa na furaha na shukrani baada ya
ushindi huo wa kihistoria. Rashid, ambaye ana umri wa miaka 21 tu,
anaishi na familia yake maeneo ya Temeke, Dar es Salaam.
Akizungumzia
ushindi wake, Rashid ambaye amemaliza kidato cha nne hivi karibuni,
alisema kuwa alikuwa anacheza angalau mara 4 hadi 6 kwa wiki kwa kutumia
pesa aliyokuwa anaipata katika shughuli zake za kila siku.
'Ndoto
yangu ni kujenga nyumba, na kuwekeza katika kilimo, kitu ambacho
nitafanya kwa kushirikiana na mama pamoja na Baba yangu. Nia yangu ni
kuikuza iwe ni biashara kubwa ' alisema Rashid.
Pia
alisema ana mpango wa kuendelea kucheza mchezo na kuwa balozi wa Tatu
Mzuka, ili kuwasaidia watu kufurahia mchezo huo na kuuamini. "Watu
wengine ni wagumu kuamini kwamba unaweza kushinda kiwango hiki kikubwa
cha fedha kupitia shilingi 500 tu. Ninafurahi kuwa miongoni mwa watu wa
kwanza kuthibitisha hili"
Balozi wa Mchezo wa Bahati Nasibu wa Tatu Mzuka, Mussa Hussein (kulia), akimkabidhi mfano wa hundi ya thamani ya shilingi milioni 80 Mshimdi Mkuu wa Mchezo huo, Rashid Ally katika hafla iliyofanyika Hoteli ya Regence Mikocheni Jijini Dar es Salaam leo. Katikati ni Mwakilishi kutoka Baraza la Michezo ya Bahati Nasibu Tanzania, Abdallah Hemed.
Meneja Masoko wa Kampuni hiyo, Lumuliko Mengele, akizungumza katika hafla hiyo. Kushoto ni mama wa mshindi huyo, Fatma Kavila. Katikati ni mshindi, Rashid Ally.
Baba, mama na mwana wakiwa wameshika mfano wa hundi wa kiasi hicho cha fedha alichoshinda mtoto wao.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...