Katibu Mkuu Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Prof.
Elisante Ole Gabriel ( kulia) akipata maelekezo kutoka kwa Mkuu wa
kituo cha Makumbusho cha Caravan Serai Bibi. Reinfrida Kapela (kushoto)
namna ambavyo wanawake wa Mji wa Bagamoyo walivyokuwa na
utamaduni wa kutengeneza urembo wa liwa kwa kutumia jiwe wakati wa
ziara yake ya kikazi jana Mjini hapo.
Katibu Mkuu Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Prof.
Elisante Ole Gabriel ( kushoto) akieleza jambo wakati wa kikao na Maafisa
Utamaduni na watendaji wa Mkoa wa Pwani katika ziara yake ya kikazi
jana mkoani hapo lengo ikiwa ni kuwahamasisha maafisa hao kufanya
kazi kwa kuzingatia utamaduni wa kutunza na kuheshimu muda ili kuleta
matokeo chanya kwa jamii kulia ni Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu
Bibi. Joyce Fisoo.
Baadhi ya wajumbe wa kikao waliohudhuria kikao kazi wakati wa
ziara ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo
Prof. Elisante Ole Gabriel Jana Mkoani Pwani.
Katibu Mkuu Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Prof.
Elisante Ole Gabriel (wa kwanza kushoto) akimsikiliza Mkuu wa kituo cha
Makumbusho cha Caravan Serai Bibi. Reinfrida Kapela (kulia) wakati wa
ziara yake ya kikazi jana Mjini Bagamoyo, katikati ni Katibu Tawala
Wilaya ya Bagamoyo Bibi. Erica Yegela.
Katibu Mkuu Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Prof.
Elisante Ole Gabriel (waliokaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na
watendaji wa Mkoa wa Pwani wakati wa ziara yake ya kikazi jana
mkoani hapo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...