JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MALIASILI NA UTALII
TAARIFA KWA UMMA
Kamati
ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Ngorongoro, kwa kushirikisha Hifadhi ya Taifa
Serengeti na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro, inaendesha zoezi la kuondoa
mifugo na makazi ndani ya hifadhi ya Taifa Serengeti na kwenye mpaka wa Pori
Tengefu Loliondo.
Zoezi
hilo lililoanza tarehe 10 Agosti 2017 litadumu kwa siku kumi na nne na linashirikisha
Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya ya Ngorongoro, Jeshi la Polisi, Usalama wa
Taifa, Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro, Hifadhi ya Taifa Serengeti na Hifadhi
ya eneo la Ngorongoro.
Zoezi
hilo linalenga kunusuru uhifadhi ndani ya hifadhi, ndani ya Pori Tengefu
Loliondo, na ndani ya mfumo ikolojia wa Serengeti na pia kunusuru utalii katika
mfumo ikolojia huo.
Aidha,
hatua hii ya kuondoa makazi na mifugo kutoka katika maeneo ya mipaka ya Pori
Tengefu Loliondo kutaongeza uhakika wa kupatikana malisho ya mifugo wakati wa
kiangazi kwa kuwa hakutakuwepo na makazi ndani ya Hifadhi na ufugaji holela.
kimsingi
zoezi hili linaendana na wito wa Serikali wa kuondoa mifugo ndani ya maeneo
yote yaliyohifadhiwa nchini.
Katika
kutekeleza zoezi hili, Mkuu wa Wilaya
Ngorongoro, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama
Wilaya ya Ngorongoro Bwana Rashidi Taka, alitoa maelekezo yafuatayo:
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...