Balozi wa Cuba nchini Tanzania, Profesa Lucas Domingo Hernandez Polledo akizungumza na baadhi ya wakurugenzi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) wakati akiitembelea leo. Kushoto ni Mratibu wa madaktari wa Cuba nchini, Dk Maylen Lopez. Kutoka kushoto wa tatu ni Mkurugenzi wa Rasilimali Watu Muhimbili, Makwaia Makani, Mkurugenzi wa Upasuaji, Dk. Julieth Magandi, ofisa Idara ya ufundi, Mkurugenzi wa Tiba, Dk. Hedwiga Swai, Mkurugenzi Mtendaji, Profesa Lawrence Museru na Mkurugenzi wa Ufundi, Gaudence Aksante.
Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Profesa Lawrence Museru akizungumza na Balozi wa Cuba nchini, Profesa Lucas Domingo Hernandez Polledo. Kulia ni Mkurugenzi wa Ufundi, Gaudence Aksante.
Balozi wa Cuba nchini, Profesa Lucas Domingo Hernandez Polledo akimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Muhimbili, Profesa Museru leo kabla ya kutembelea maeneo ya kutoa huduma katika hospitali hiyo.
Balozi wa Cuba na baadhi ya wafanyakazi wa hospitali hiyo wakiwa katika chumba cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalumu (ICU).
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...