Na Benedict Liwenga-WHUSM.
Waziri
wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe
kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Prof. John Palamagamba
amezindua Mpango wa Usajili na Utoaji Vyeti kwa Watoto waliochini ya
Umri Miaka Mitano kwa Mikoa ya Mtwara na Lindi.
Uzinduzi
huo umefanyika leo katika Viwanja vya Matogolo Wilayani Tandahimba
Mkoani Mtwara ukiwa na lengo la kuwasajili watoto waliochini ya umri
miaka mitano pamoja na kuwapatia vyeti ambavyo vitawasaidia kutambulika
kwao na kisha kupewa nyaraka za uthibitisho yaani vyeti vya kuzaliwa.
Waziri
Mwakyembe amesema kwamba, katika kupanga maendeleo ya nchi kunahitajika
takwimu sahihi za matukio muhimu za Watanzania ambazo zinaelezea
taarifa zao za kuzaliwa ikiwemo za vifo kwakuwa takwimu hizo zinasaidia
kujua mahitaji ya wananchi katika sekta mbalimbali ikiwemo afya, elimu,
lishe pamoja na sehemu nyinginezo.
“Mpango
huu utaondoa utegemezi wa takwimu za kuhisia, takwimu za kukadilia
ndugu zangu mfumo tulionao sasa unategemea Sensa ambayo hufanyika kila
baada ya miaka 10, na matukio bado yanatokea, hivyo kutumia Mpango huu
kutasaidia kupata takwimu sahihi na halisi za Watanzania wote”, alisema,
Dkt. Mwakyembe.
Ameongeza
kuwa, Mikoa ya Lindi na Mtwara itanufaika na mpango huo kwakuwa
Serikali itakuwa inatambua mahitaji halisi ya wananchi kupitia taarifa
zitakazochukuliwa za uandikishaji wa watoto hao, huku akisisitiza kuwa,
anaamini kwamba mikoa hiyo itakuwa chachu ya kuongezeka kwa idadi ya
watoto watakaoandikishwa kama ilivyofanyika katika baadhi ya mikoa
mingine ya Tanzania.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe akiongea na Wakazi wa Wilaya ya Tandahimba Mkoani Mtwara (hawapo pichani) wakati wa Uzinduzi wa Mpango wa Usajili na Utoaji Vyeti kwa Watoto waliochini ya Umri Miaka Mitano kwa Mikoa ya Lindi na Mtwara leo 26 Septemba, 2017.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe akikata utepe katika Kitabu cha Usajili pamoja na Simu kuashiria Uzinduzi wa Mpango wa Usajili na Utoaji Vyeti kwa Watoto waliochini ya Umri Miaka Mitano kwa Mikoa ya Lindi na Mtwara leo 26 Septemba, 2017.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe akiwa katika picha ya pamoja na Wadau mbalimbali wanaosaidia Mpango wa Usajili na Utoaji Vyeti kwa Watoto waliochini ya Umri Miaka Mitano mara baada ya kuuzindua leo Wialayani Tandahimba, Mkoani Mtwara, 26 Septemba, 2017.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (aliyevaa kofia ya pama) akiwakabidhi vyeti Wazazi kwa niaba ya watoto wao wenye umri chini ya miaka mitano wakati wa Uzinduzi wa Mpango wa Usajili na Utoaji Vyeti kwa Watoto waliochini ya Umri Miaka Mitano leo Wilayani Tandahimba, Mkoani Mtwara 26 Septemba, 2017.
PICHA ZOTE NA BENEDICT LIWENGA-WHUSM
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...