NI ukweli usiopingika utekelezaji wa sekta ya viwanda inahitaji
nishati ya umeme katika shughuli zake mbalimbali ikiwemo za uzalishaji mali ili kuweza kupata mafaniko yanayoweza kusaidia kuinua uchumi wao.

Kwani bila kuwepo kwa nishati hiyo kwa baadhi ya maeneo hasa vijijini kuna pelekea kushindwa kufikia malengo yao kwa kuongeza uzalishaji wa bidhaa mbalimbali kwa kuhofia iwapo zitakaa muda mrefu zitaharibika.Licha ya hivyo lakini pia kukosekana kwa nishati hiyo kuna sababisha watanzania wenye nia ya kuanzisha viwanda vidogo vidogo kukwama kufikia malengo yao waliojiwekea kwa kuvianzisha.

Kufuatia kuwepo kwa changamoto hiyo, Shirika la Umoja wa Mataifa la Mfuko wa Mitaji na Maendeleo (The United Nations Capital Development Fund –UNCDF) kwa kushirikiana na kampuni ya Ensol Tanzania Limited waliamua kuanzisha mradi wa umeme wa jua (sola) kwenye kijiji cha Mpale Kata ya Mpale wilayani Korogwe Mkoani Tanga.

Mradi huo ambao umekuwa mkombozi mkubwa kwa wananchi wa Kijiji hicho umefadhiliwa na Shirika hilo ambao umelenga kuwasaidia kuondokana na changamoto ambazo zilikuwa zikiwakabili ikiwemo kutumia vibatari wakati wakienda kujifungua kwenye zahanati ya Kata hiyo.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini,Dkt Juliana Pallangyo akizundua mradi huo 
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini,Dkt Juliana Pallangyo kushoto akipata maelezo ya mradi huo mara baada ya kutembelea kwenye eneo la mtambo huo kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Korogwe Mkoani Tanga,Mhandisi,Robert Gabriel.


Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini,Dkt Juliana Pallangyo akishiriki kucheza ngoma ya wananchi wa Kijiji hicho mara baada ya kuzinduaa mradi huo .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...