Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii
MKUU wa
Wilaya ya Same, Rosemary Senyamule ameigiza Tanesco Same kuwafata wateja
popote walipo hili kuongeza kasi ya huduma kwa kuhakikisha kuwa kila mahali
wanapata Umeme.
Dc Sinyamule
amesema hayo alipokuwa akizindua tawi la Tanesco Hedaru na Kisiwani katika Wilaya Same na kumbusha kuongeza ofisi
maeneo ya milimani.
“Kuhakikisha mkandarasi anayefanya
kazi kuzingatia uimara wa nguzo hasa maeneo ya milimani pamoja na Kutengeneza
mabango yanayoonyesha wateja tahadhari za kuchukua juu ya umeme ili kupunguza
madhara ya vifaa na umeme kukatikakatika”Amesema Dc Sinyamule.
Amewataka Kuhakikisha wanaendelea kutoa huduma
kwa haraka na Kuanzisha na kuitangaza namba ya simu ya mkononi kwa ajili ya
wateja.
Pia
aliwakumbusha wateja kuongeza kasi ya kuweka umeme na kulipia huduma za umeme pindi watakapohitajika
kuunganishiwa.
Pia
aliwakumbusha kuanza kutumia umeme kwa uchumi kwa kuanzisha viwanda vidogo na
vya kati kwani serikali imekusudia kumaliza tatizo la umeme ifakapo 2021.
Kwa Upande wake Meneja wa Tanesco Kanda ya
Kaskazini, Mhandisi Hiza amesema shirika limejipanga kusogeza huduma karibu
baada ya ongezeko kubwa la wateja wanaotokana na mpango wa serikali REA.
Hivyo
aliwaomba wakazi wa Wilaya ya Same na Vitongoji vyake Kulipa bili kwa wakati na kutumia
umeme kwa uangalifu ili kusiwepo umeme unaopotea bila sababu.
Aidha aliwaomba
wakazi wa eneo hilo Kuchukua
tahadhari za usalama pamoja na kutunza miundombinu na Kutoa taarifa haraka
kunapotokea tatizo/ uharibifu
Mkuu wa Wilaya ya Same Rosemary Sinyamule akikata utepe wakati wa uzinduzi wa Ofisi ya Tanesco Hedaru wilayani Same Mkoa wa KilimanjaroMkuu wa Wilaya ya Same, Rosemary Sinyamule akizungumza na wadau mara baada ya kufungua ofisi ya Tanesco Hedaru
Mkuu wa Wilaya ya Same, Rosemary Sinyamule akiwa katika picha ya pamoja Wafanyakazi wa Tanesco Hedaru
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...