Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii
MKUU wa Wilaya ya Same, Rosemary Senyamule ameigiza  Tanesco Same  kuwafata wateja popote walipo hili kuongeza kasi ya huduma kwa kuhakikisha kuwa kila mahali wanapata Umeme.

Dc Sinyamule amesema hayo alipokuwa akizindua tawi la  Tanesco  Hedaru na Kisiwani katika Wilaya Same na kumbusha kuongeza ofisi maeneo ya milimani.

Kuhakikisha mkandarasi anayefanya kazi kuzingatia uimara wa nguzo hasa maeneo ya milimani pamoja na Kutengeneza mabango yanayoonyesha wateja tahadhari za kuchukua juu ya umeme ili kupunguza madhara ya vifaa na umeme kukatikakatika”Amesema Dc Sinyamule.

Amewataka Kuhakikisha wanaendelea kutoa huduma kwa haraka na Kuanzisha na kuitangaza namba ya simu ya mkononi kwa ajili ya wateja.
Pia aliwakumbusha wateja kuongeza kasi ya kuweka umeme na  kulipia huduma za umeme pindi watakapohitajika kuunganishiwa.

Pia aliwakumbusha kuanza kutumia umeme kwa uchumi kwa kuanzisha viwanda vidogo na vya kati kwani serikali imekusudia kumaliza tatizo la umeme ifakapo 2021.

 Kwa Upande wake Meneja wa Tanesco Kanda ya Kaskazini, Mhandisi Hiza amesema shirika limejipanga kusogeza huduma karibu baada ya ongezeko kubwa la wateja wanaotokana na mpango wa serikali  REA.

Hivyo aliwaomba wakazi wa Wilaya ya Same na Vitongoji vyake Kulipa bili kwa wakati na kutumia umeme kwa uangalifu ili kusiwepo umeme unaopotea bila sababu.

Aidha aliwaomba wakazi wa eneo hilo Kuchukua tahadhari za usalama pamoja na kutunza miundombinu na Kutoa taarifa haraka kunapotokea tatizo/ uharibifu
 Mkuu wa Wilaya ya Same Rosemary Sinyamule akikata utepe wakati wa uzinduzi wa Ofisi ya Tanesco Hedaru wilayani Same Mkoa wa Kilimanjaro
 Mkuu wa Wilaya ya Same, Rosemary Sinyamule  akizungumza na wadau mara baada ya kufungua ofisi ya Tanesco Hedaru
Mkuu wa Wilaya ya Same, Rosemary Sinyamule akiwa katika picha ya pamoja Wafanyakazi wa Tanesco Hedaru

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...