Mkuu wa Magereza Mkoa wa Morogoro, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Mzee Nyamka (kushoto), pamoja na Maafisa wengine wa Jeshi hilo, wakitoka katika Gereza la Kilimo Idete lililopo Ifakara, mara bada ya Naibu Waziri huyo kupokeataarifa ya Ujenzi wa Mradi wa Umwagiliaji uliosimama baada ya Mkandarasi kuutelekeza mradi huo wenye thamani ya shilingi Bilioni 2.5. Hata hivyo, Masauni alilitaka Jeshi hilo kufanya uchunguzi dhidi ya Mkandarasi huyo na ikithibitika anamakosa akamatwe na achukuliwe hatua za kisheria.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni(kulia),
Karani wa Ujenzi wa Mradi wa Umwagiliaji wa Gereza la Kilimo Idete, Ifakara, Mkaguzi wa Jeshi la Magereza, Juma Mtega, akimuonyesha Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kushoto),chanzo cha ujenzi wa mradi huo. Masauni alifanya ukaguzi wa mradi huo wa mabilioni ya fedha ambao Mkandarasi aliutelekeza mwaka 2016. Hata hivyo, Masauni alilitaka Jeshi la Magereza kufanya uchunguzi dhidi ya Mkandarasi huyo na ikithibitika anamakosa akamatwe na achukuliwe hatua za kisheria.
Mkuu wa Jeshi la Magereza Mkoa wa Morogoro, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Mzee Nyamka, akimuonyesha Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kulia), sehemu mbalimbali za Ujenzi wa Mradi wa Umwagiliaji wa Gereza la Kilimo Idete, Ifakara, wakati Masauni alipofanya ziara ya ukaguzi wa ujenzi huo wa zaidi ya shilingi Bilioni 2.5 uliosimama baada ya Mkandarasi wa mradi huo, kuutelekeza mwaka 2016. Hata hivyo, Masauni alilitaka Jeshi hilo kufanya uchunguzi dhidi ya Mkandarasi huyo na ikithibitika anamakosa akamatwe na achukuliwe hatua za kisheria.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kulia), akitoa maelekezo kwa viongozi wa Jeshi la Magereza Mkoa wa Morogoro ya kumchunguza na kumchukulia hatua za kisheria endapo itathibitika Mkandarasi aliyesimamisha Ujenzi wa Mradi wa Umwagiliaji wa Gereza la Kilimo Idete, Ifakara, alifanya makosa kwa kusimamisha ujenzi wa mradi huo wa mabilioni ya fedha, tangu mwaka jana 2016. Wapili kushoto ni Mkuu wa Magereza Mkoa wa Mkoa huo, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Mzee Nyamka.


KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...