Na Mwandishi wetu.
Mashindano
ya kumsaka mrembo wa Kiss Universe Tanzania yamepangwa kufanyika Jumamosi kwenye ukumbi
wa Makumbusho ya Taifa jijini.
Mashindano hayo
yatashirikisha jumla ya warembo 10 kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania Bara kwa
mujibu Mkurugenzi wa Kampuni ya Compass Communications, Maria Tsehai Sarungi.
Maria
amewataja mabondia hao kuwa ni Lilian Maraule , Glory Gideon, Melody Tryphone,
Anitha Mlay, Silvia Mkomwa, Rogathe Ally, Prisca Dastan ambao wote wanatoka Dar
es Salaam.
Warembo
wengine ni Maureen Foster na Mary Peter wanaotoka Mwanza wakati anayetoka mkoa
wa Mbeya Zahra Abdul.
Alisema kuwa
warembo hao watakuwa chini ya Miss Universe namba mbili wa mwaka jana, Lilian
Loth katika kambi ya mashindano hayo yaliyodhaminiwa na SeaCliff Court Residence,
Diana Magese, MnM, Kasakana na Bonuzi.
“Maandalizi
ya mashindano hayo yamekamilika na wapenzi
wa masuala ya urembo watapata burudani safi kutoka kwa DDI Dance, poetry group (Romantic), A
beautiful song kutoka kwa Jeff Mduma,”
alisema Maria.
Alifafanua kuwa
wamedhamilia kumpata mrembo bora ambaye atarejesha heshima ya mashindano hayo
kama ilivyokuwa kwa Flaviana Matata ambaye alimaliza katika nafasi tano bora
nchini Mexico mwaka 2007.
“Tumefanya
uchaguzi wa warembo vizuri na wengi ni bora, kwa sasa tunawafundisha masuala
mbalimbali ya urembo, lengo ni kuwafanya wawe bora, wote ni washindi, lakini
tunahitaji mshindi mmoja ambaye ataliwakilisha Taifa katika mashindano ya Kimataifa,”
alisema.
Alisema kuwa
mashindano hayo pia yatamtoa mshindi wa taji la Miss Earth Tanzania na mshindi
wa taji la Miss Tourism Queen International wa Tanzania.
Washiriki wa shindano la ulimbwende la Miss Universe wakijipodoa katika kambi yao ya SeaCliff Residence iliyopo Masaki jijini.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...